Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Watu wengine huona kwamba Yesu ndiye mtu mkuu zaidi katika historia. Wengine hutilia shaka kama kweli aliwahi kuishi. Je, wafikiri ni muhimu kumwamini? [Baada ya jibu, soma Matendo 4:12.] Kuna uthibitisho gani kwamba kweli Yesu aliwahi kuishi duniani? Gazeti hili lajibu swali hilo.”
Amkeni! Juni 22
“Watu wengi wanahangaika sana kuhusu mazingira. Je, wafikiri kwamba inawezekana kuhifadhi misitu ya mvua ulimwenguni? [Ngoja jibu.] Gazeti hili laeleza jitihada ambazo zimefanywa hivi karibuni ili kuokoa misitu ya mvua. Pia lazungumzia jinsi ahadi hiyo nzuri ya Mungu itakavyotimizwa.” Soma Isaya 11:9.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Mojawapo ya mahitaji yetu ya msingi tukiwa wanadamu ni kupenda na kupendwa. [Soma maelezo ya picha iliyo kwenye ukurasa wa 4.] Lakini, je umegundua kwamba jamii ya sasa hupenda kutanguliza mambo mengine? [Ngoja jibu.] Gazeti hili lazungumzia upendo wa kweli na jinsi ya kuustawisha.” Soma 1 Wakorintho 13:2.
Amkeni! Julai 8
“Watu wengi wanasumbuliwa na ongezeko la jeuri. [Taja mfano mmoja unaojulikana kwenu, na ungoje jibu.] Gazeti hili lachunguza baadhi ya mambo yanayosababisha jeuri. Pia laeleza jinsi Mungu atakavyokomesha uhalifu na jeuri kabisa.” Soma Zaburi 37:10, 11.