Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Unafikiri kuna wakati ambapo hakutakuwa na umaskini ulimwenguni? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi ya Mungu. [Soma Isaya 65:21.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi ahadi hiyo ya Mungu itakavyotimia.” Panga kumrudia ili ujibu swali hili: Ahadi hiyo itatimizwa lini?
Amkeni! Mei 22
“Watu wengi wanajua kwamba mazoezi ni muhimu kwa afya, hata hivyo wengi wanakiri kwamba hawafanyi mazoezi ya kutosha. Je, ndivyo ilivyo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia manufaa ya kufanya mazoezi kwa ukawaida na lina mapendekezo kuhusu jinsi tunavyoweza kufanya mazoezi licha ya shughuli nyingi tulizo nazo.”
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Ijapokuwa karibu kila mtu huzungumzia amani, wanadamu wameshindwa kutokeza umoja ulimwenguni. Je, unafikiri kwamba kupatikana kwa amani ulimwenguni ni ndoto tu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia serikali inayoweza kuunganisha ulimwengu.” Soma Zaburi 72:7, 8, na upange kurudi ili kuzungumzia jinsi hilo litakavyotimizwa.
Amkeni! Juni 8
“Je, umeona kwamba watu wengi wanahangaishwa na kuongezeka kwa ugonjwa wa kansa ya ngozi? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! laeleza ni kwa nini leo tumo hatarini hata zaidi na jinsi tunavyoweza kujikinga.” Malizia kwa kuzungumzia ahadi yenye kufariji iliyo katika Ayubu 33:25.