Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Kila siku tunasikia ripoti za jeuri. Je, wafikiri hali hizo zilikuwapo zamani? [Ngoja jibu.] Hebu ona jinsi Biblia inavyosema. [Soma Mathayo 24:37.] Siku za Noa zilikuwa mbaya sana hivi kwamba Mungu akawaangamiza watu wote isipokuwa Noa na familia yake. Gazeti hili linaonyesha maana ya matukio hayo kwetu leo.”
Amkeni! Mei 22
“Leo, magonjwa yanayoenezwa na wadudu ni mojawapo ya hatari nyingi kwa afya yetu. Je, wajua kwamba tunaweza kuchukua hatua fulani ili kujikinga? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia hatua hizo, vilevile ahadi ya Biblia ya wakati ambapo hakutakuwa na magonjwa tena.” Malizia kwa kusoma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Ripoti kuhusu matumizi mabaya ya pesa za misaada zimewafanya watu fulani wajiulize kama inafaa kutoa michango kwa mashirika ya misaada. Hata hivyo, watu wengi sana wana uhitaji. Unafikiri ni jambo gani linaloweza kufanywa? [Ngoja jibu. Kisha soma Waebrania 13:16.] Gazeti hili linaeleza utoaji unaompendeza Mungu.”
Amkeni! Juni 8
“Inaonekana kwamba watu leo hawajali maadili na adabu kama zamani. Je, umejionea jambo hilo? [Ngoja jibu.] Biblia ilitabiri jambo hilo. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili la Amkeni! linaeleza kwa nini maadili ya wanadamu yanabadilika, na tumaini la wakati ujao.”