Barua ya Ofisi ya Tawi
Wahubiri wa Ufalme Wapendwa:
“Mungu akafuliza kuikuza.” (1 Kor. 3:6) Inafurahisha sana kuona ukuzi mkubwa katika Afrika Mashariki! Katika mwaka wa utumishi wa 2003, mafunzo mapya ya Biblia zaidi ya 6,000 yalianzishwa! Mnastahili pongezi.
Yehova anabariki utendaji katika maeneo ya mbali. Makutaniko au vikundi vimeanzishwa sehemu mbalimbali na habari njema zinafikia maeneo ya mbali sana ya eneo letu lenye matokeo.—Mt. 24:14.
Ili kuandaa vichapo kwa ajili ya shamba linaloendelea kuongezeka ulimwenguni pote, Matbaa iliyo katika Watchtower Farms, karibu na Wallkill, New York, inapanuliwa. Kazi ya kupanua jengo hilo kwa ekari tatu na nusu inaendelea. Upanuzi huo unalingana na eneo la Majumba ya Ufalme 30 ya wastani! Mashine mbili kubwa za kisasa za kuchapa zitawasili mwanzoni mwa mwaka wa 2004. Kila mashine itakuwa na uwezo wa kuchapa magazeti 25 hivi kwa sekunde. Mashine mpya za kujalidi na kupakia zitawekwa pia katika mwaka wa 2004. Kazi nyingi zaidi itafanywa na wafanyakazi wachache.
Tunapoingia katika mwaka wa utumishi wa 2004, tunaungana nanyi kusali kwamba Yehova ‘atafuliza kuikuza.’
Ndugu zenu,
Ofisi ya Tawi ya Kenya