Sanduku La Swali
◼ Je, funzo la Biblia la familia linapaswa kuripotiwa?
Ikiwa mzazi Mkristo anaongoza funzo la Biblia la familia na watoto wasiobatizwa wanashiriki, mzazi huyo anaweza kuripoti saa moja tu kwa juma, rudio moja kwa juma, na funzo moja la Biblia kila mwezi. Atafanya hivyo hata kama funzo linachukua zaidi ya saa moja, au linaongozwa zaidi ya mara moja kwa juma, au kama anajifunza na mtoto mmoja-mmoja.—Ona kitabu Huduma Yetu, uku. 104.
Ikiwa kila mtu katika familia amebatizwa, basi hataripoti saa wala funzo (lakini ataripoti ikiwa mtoto mmoja bado anajifunza kitabu cha pili baada ya ubatizo). Atafuata utaratibu huo kwa sababu ripoti ya kutaniko ya utumishi wa shambani inahusu hasa kazi ya kuhubiri habari njema na kuwafundisha kweli ya Biblia watu ambao hawajajiweka wakfu na kubatizwa. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Hata hivyo, jambo hilo halipunguzi umuhimu wa kuongoza funzo la familia kwa ukawaida.
Ni wajibu wa wazazi Wakristo kujifunza na watoto wao. Wale wanaohitaji msaada wa kuanzisha au kuboresha funzo lao la familia wanaweza kuwaomba wazee msaada. Ikiwa inafaa mhubiri mwingine ajifunze Biblia na mwana au binti asiyebatizwa ambaye ana wazazi Wakristo kutanikoni, mwangalizi msimamizi au mwangalizi wa utumishi anapaswa kuulizwa. Funzo hilo likiidhinishwa, yule ambaye analiongoza anaweza kuliripoti kama anavyoripoti mafunzo mengine ya Biblia.
Kuwazoeza watoto katika njia za Yehova kunahitaji wakati na jitihada nyingi zaidi kuliko ripoti ya utumishi inavyoonyesha. (Kum. 6:6-9; Met. 22:6) Wazazi Wakristo wanastahili pongezi kwa sababu ya kutimiza wajibu wao mzito wa kuwalea watoto wao “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.”—Efe. 6:4.