Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 8
  • Kwa Nini Funzo la Kitabu la Kutaniko Ni Muhimu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Funzo la Kitabu la Kutaniko Ni Muhimu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Ambavyo Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Hutusaidia
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu Binafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Msaada Wakati Unaofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Jinsi ya Kunufaika Kutokana na Kikundi Chako cha Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 8

Kwa Nini Funzo la Kitabu la Kutaniko Ni Muhimu?

1 Katika mwaka wa 1895, vikundi vya funzo vya Wanafunzi wa Biblia, kama Mashahidi wa Yehova walivyoitwa wakati huo, viliitwa Vikundi vya Mapambazuko kwa Ajili ya Funzo la Biblia. Mabuku ya Millennial Dawn yalitumiwa kwa ajili ya funzo. Baadaye mikutano hiyo ikaitwa Vikundi vya Kiberoya kwa Ajili ya Funzo la Biblia. (Mdo. 17:11) Mara nyingi vikundi vidogo-vidogo vilikutana katika nyumba za faragha, wakati wa jioni uliowafaa washiriki. Hivyo ndivyo Funzo la Kitabu la Kutaniko lilivyoanza.

2 Kitia-Moyo na Msaada: Kwa kuwa vikundi vya funzo la kitabu vinakusudiwa viwe vidogo-vidogo, kuna nafasi zaidi kwa wahudhuriaji kuonyesha imani yao kwa kutoa maelezo. Hilo hutokeza “ubadilishanaji wa kitia-moyo . . . , kila mmoja kupitia imani ya mwingine.”—Rom. 1:12.

3 Kuangalia jinsi mwangalizi wa funzo la kitabu anavyofundisha kunaweza kutusaidia ‘tulitumie sawasawa neno la kweli.’ (2 Tim. 2:15) Angalia jinsi anavyokazia msingi wa Kimaandiko wa habari hizo. Ikitegemea kitabu cha funzo, anaweza kukazia mambo makuu kwa kuyarudia mwishoni mwa funzo, akitumia Biblia pekee. Mfano wake mwema unaweza kutusaidia tuboreshe ufundishaji wetu katika huduma ya shambani.—1 Kor. 11:1.

4 Zaidi ya kuongoza funzo la kila juma, mwangalizi wa funzo la kitabu huongoza katika kazi ya kuhubiri. Yeye hufanya mipango hususa ya utumishi wa shambani akishirikiana na mwangalizi wa utumishi. Yeye hujitahidi kuwasaidia wote katika kikundi chake watimize wajibu wao wa Kikristo wa kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi.—Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 9:16.

5 Mwangalizi wa funzo la kitabu hupendezwa na hali ya kiroho ya kila mmoja katika kikundi. Yeye huonyesha upendezi huo kwenye mikutano ya kutaniko na anapohubiri na wengine katika utumishi wa shambani. Anapopata nafasi ya kuwatembelea akina ndugu nyumbani mwao, yeye pia hutumia nafasi hiyo kuwatia moyo kiroho. Wote na wawe huru kumwendea mwangalizi wa funzo la kitabu ili wapate msaada wa kiroho wakati wowote wanapouhitaji.—Isa. 32:1, 2.

6 Kutiana Nguvu: Katika nchi ambazo kazi ya watu wa Mungu imewekewa vizuizi, mara nyingi akina ndugu hukutana katika vikundi vidogo-vidogo. Ndugu mmoja alisema hivi: “Hata ingawa utendaji wetu wa Kikristo ulikuwa umepigwa marufuku, ilipowezekana tulifanya mikutano yetu ya kila juma katika vikundi vya watu 10 hadi 15. Mikutano hiyo ilitutia nguvu kiroho, kupitia funzo letu la Biblia na ushirika wetu baada ya funzo. Tulisimuliana mambo yaliyoonwa, na hayo yalitusaidia kutambua kwamba kila mmoja wetu alikuwa na magumu yaleyale.” (1 Pet. 5:9) Vivyo hivyo, sisi pia na tutiane nguvu kwa kuunga mkono kikamili mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko.—Efe. 4:16.

[Maswali ya Funzo]

1. Mipango ya Funzo la Kitabu la Kutaniko ilianzaje?

2. Tunaweza kuchangiaje “ubadilishanaji wa kitia-moyo” kwenye funzo la kitabu?

3, 4. Mpango wa funzo la kitabu hutusaidiaje kutimiza huduma yetu?

5. Tunaweza kupata msaada gani kupitia funzo la kitabu?

6. (a) Ndugu zetu katika nchi fulani wametiwaje nguvu kwa kukutana katika vikundi vidogo-vidogo? (b) Wewe binafsi umefaidikaje na mpango wa funzo la kitabu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki