Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 4
  • Kutoa Ushahidi Bila Kusema Neno Lolote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Ushahidi Bila Kusema Neno Lolote
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Matendo Mema Yamtukuzayo Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Onyesha kwa Matendo Kwamba Wewe Ni Shahidi wa “Habari Njema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 4

Kutoa Ushahidi Bila Kusema Neno Lolote

1 Uumbaji wa Yehova hufunua mengi sana kuhusu sifa zake zisizoonekana bila kusema neno lolote. (Zab. 19:1-3; Rom. 1:20) Vivyo hivyo, mwenendo wetu mzuri, sifa zetu za Kikristo, na sura yetu nzuri hutoa ushahidi bila maneno. (1 Pet. 2:12; 3:1-4) Kila mmoja wetu anapaswa kuwa na hamu ya ‘kulipamba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote’ kupitia mwenendo wetu.—Tito 2:10.

2 Wanadamu wasio wakamilifu wanawezaje kufanya mafundisho ya Biblia yavutie? Hilo linawezekana tu kupitia mwongozo wa Neno la Mungu na nguvu za roho takatifu. (Zab. 119:105; 143:10) Neno la Mungu “liko hai nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili.” (Ebr. 4:12) Linapenya ndani sana katika mioyo yetu na kutuwezesha kujivika utu mpya. (Kol. 3:9, 10) Tukiwa na roho takatifu tunadhihirisha sifa zenye kuvutia kama vile fadhili, wema, upole, na kujizuia. (Gal. 5:22, 23) Je, sisi binafsi tunaruhusu neno la Mungu na roho yake ituongoze maishani?—Efe. 4:30; 1 The. 2:13.

3 Wengine Wanatuona: Tunapofuata viwango vya Yehova maishani mwetu na kujitahidi kuonyesha sifa zake, wengine wanatuona. Kwa mfano, fikiria mtu fulani ambaye alidhihakiwa na wafanyakazi wenzake kwa sababu yeye ni mfupi. Dada aliyefanya kazi katika ofisi hiyo alimheshimu mtu huyo na kumtendea kwa fadhili sikuzote. Jambo hilo lilimfanya amuulize dada huyo kwa nini ilimtendea kwa njia tofauti. Dada yetu alimwambia kwamba alimtendea kwa heshima kwa sababu ya kufuata kanuni za Biblia katika maisha yake. Vilevile alimhubiria kuhusu tumaini zuri la Ufalme. Mtu huyo alianza kujifunza Biblia na mwishowe akafanya maendeleo na kubatizwa. Aliporudi katika nchi yao, watu wa ukoo walivutiwa na mwenendo wake mzuri na baadhi yao wakakubali kweli.

4 Tunapokuwa kazini, shuleni, au tunaposhughulika na watu wa ukoo na majirani wetu, mwenendo wetu mzuri, pamoja na ushahidi wetu unaweza kuwachochea wengine wampe Mungu utukufu.—Mt. 5:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki