Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Watu duniani kote wamesikia kumhusu Yesu Kristo. Baadhi yao husema kwamba yeye ni mtu wa pekee tu. Wengine humwabudu kama Mungu Mweza Yote. Wewe unafikiri Yesu Kristo ni nani? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kinaganaga Yesu ni nani, alitoka wapi, na mahali alipo sasa.” Soma Yohana 17:3.
Amkeni! Sept. 22
“Watu wengi hawawezi kugharimia mahali pazuri pa kuishi. Je, unafikiri kwamba kuna wakati ambapo kila mtu atakuwa na nyumba nzuri? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia habari ya hivi karibuni kuhusu matatizo ya kupata makao. Pia linaonyesha kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba ahadi hii ya Mungu itatimizwa.” Soma Isaya 65:21, 22.
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
Soma swali lililo kwenye jalada, kisha uulize: “Je, unajua ni ishara gani inayorejelewa hapa? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 24:3.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mambo matano muhimu ambayo ni sehemu ya ishara hiyo na linaeleza ni kwa nini tunahitaji kuitambua.” Onyesha sanduku kwenye ukurasa wa 6.
Amkeni! Okt. 8
“Kutumia kileo vibaya husababisha matatizo mengi. Gazeti hili linaonyesha jinsi ambavyo kileo huathiri mwili. [Onyesha picha kwenye ukurasa wa 7.] Makala hizi zinazungumzia jinsi watu wanavyoweza kuacha kutumia kileo vibaya na jinsi wengine wanavyoweza kuwasaidia.”