Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/06 uku. 1
  • Tafuta Nafasi za Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tafuta Nafasi za Kuhubiri
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Kufanyiza Fursa za Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Msifu Yehova Kila Siku
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Usisahau Kamwe Wewe Ni Shahidi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 2/06 uku. 1

Tafuta Nafasi za Kuhubiri

1 Kutaniko la Kikristo lina watu wa hali mbalimbali. Hata hivyo, tumeazimia kumsifu Yehova kwa umoja. (Zab. 79:13) Tunawezaje kutafuta nafasi za kuhubiri ikiwa afya mbaya au matatizo mengine yanatuzuia kuhubiri habari njema kikamili?

2 Katika Shughuli za Kila Siku: Yesu aliwahubiria watu hata alipokuwa katika shughuli zake za kila siku. Alipokuwa akipita nje ya ofisi ya kodi alimhubiria Mathayo, alipokuwa akisafiri akamhubiria Zakayo, na alipokuwa akipumzika akamhubiria mwanamke Msamaria. (Mt. 9:9; Luka 19:1-5; Yoh. 4:6-10) Sisi pia tunaweza kuwahubiria watu tunaokutana nao katika shughuli zetu za kila siku. Tukiwa na Biblia, trakti au broshua karibu, tutakuwa tayari kuzungumza kuhusu tumaini letu.—1 Pet. 3:15.

3 Je, kushindwa kutembea kumekuzuia kwa kadiri fulani kushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba? Tafuta nafasi za kuwahubiria wahudumu wa afya na watu wengine wanaokutembelea. (Mdo. 28:30, 31) Ikiwa kwa sababu ya hali fulani unakaa nyumbani kwa muda mrefu, je, umejaribu kuhubiri kupitia simu au barua? Dada mmoja huwaandikia barua kwa ukawaida watu wa ukoo ambao si Mashahidi. Yeye hutia ndani Maandiko yenye kutia moyo na mambo aliyoona alipokuwa akihubiri.

4 Kazini au Shuleni: Tamaa yetu ya kumsifu Yehova itatuchochea pia tutafute nafasi za kupanda mbegu za kweli kazini au shuleni. Mhubiri mmoja mwenye umri wa miaka minane aliwaeleza wanadarasa wenzake mambo aliyosoma kwenye gazeti moja la Amkeni! lililokuwa likizungumza kuhusu mwezi. Baada ya kujua chanzo cha habari hiyo, mwalimu wake alianza kuchukua magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa ukawaida. Tukiwa kazini, tunaweza kuweka kitabu Biblia Inafundisha mahali ambapo wengine wanaweza kukiona. Jambo hilo linaweza kuwafanya waulize maswali na kutupa nafasi ya kuwahubiria.

5 Je, unaweza kufikiria njia za kutafuta nafasi ya kuhubiri unapokuwa katika shughuli zako za kila siku? Kwa kutumia kila nafasi tunayopata, na tujitahidi kila siku ‘kumtolea Mungu dhabihu ya sifa.’—Ebr. 13:15.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki