Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Julai 15
“Je, unafikiri siku fulani kutakuwa na serikali inayotatua matatizo ya wanadamu? [Mruhusu ajibu.] Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kusali kwa ajili ya serikali kama hiyo aliposema maneno yaliyo katika Mathayo 6:9, 10. [Soma.] Gazeti hili linaeleza jambo linalofanya Ufalme wa Mungu uwe na mamlaka zaidi ya serikali za wanadamu na linafafanua baraka ambazo ufalme huo utawaletea wanadamu.”
Amkeni! Julai
Unapokutana na kijana, unaweza kusema: “Vijana wengi wenye umri kama wako wanafikiria kuhusu ndoa. Unafikiri unaweza kupata wapi habari yenye kutegemeka kuhusu jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Hebu ona ni nani aliyeanzisha ndoa. [Soma Mathayo 19:6.] Gazeti hili linataja kanuni fulani za Biblia zinazoweza kutusaidia kuwa na ndoa yenye furaha.”
Mnara wa Mlinzi Ago. 1
“Ni jambo la kawaida leo kuwaona watu wakiwadhulumu wengine. Je, unafikiri mambo yangebadilika iwapo watu wangetii maneno haya ya Yesu? [Soma Mathayo 7:12. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha kutoka kwa Biblia jinsi wanadamu wote watakavyopata haki yao ya msingi ya heshima ya binadamu.”
Amkeni! Ago.
“Sisi sote hutaka matibabu mazuri. Je, unajua kwamba madaktari wengi leo husita kuwatia watu damu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza sababu inayowafanya wahisi hivyo. Pia, linaeleza sababu kutoka katika Biblia zinazomfanya Mungu aione damu kuwa yenye thamani.” Soma Mambo ya Walawi 17:11.