Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
Yehova anastahili kutukuzwa. Sisi humtukuzaje Yehova? Wengine wanakabili matatizo gani wanapofanya hivyo? Wale wanaomtukuza Mungu wanapata faida gani sasa? Programu ya kusanyiko la mzunguko ya mwaka wa utumishi wa 2008 itatoa majibu yenye kuridhisha kwa maswali hayo. Kusanyiko hilo lina kichwa “Fanyeni Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.” (1 Kor. 10:31) Hebu ona mambo tunayotazamia katika siku mbili za kusanyiko hilo lenye maagizo mengi ya kiroho.
Mwangalizi wa wilaya atatoa hotuba zenye kichwa, “Kwa Nini Umpe Mungu Utukufu?” na “Uwe Mfano Mzuri Katika Kutimiza Matakwa ya Mungu.” Pia atatoa hotuba ya watu wote, “Ni Nani Wanaomtukuza Mungu?,” na hotuba ya mwisho, “Kumtukuza Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote.” Vilevile ataongoza Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Mwangalizi wa mzunguko atatoa hotuba zenye kichwa, “Furahia Kuangaza Utukufu wa Mungu,” “Kuzingatia Mahitaji ya Mzunguko,” na “Baki Ukiwa ‘Umewekwa Imara Katika Kweli,’” ambayo inategemea 2 Petro 1:12. Isitoshe, tutajifunza jinsi ambavyo “Huduma ya Upainia Inamtukuza Mungu.” Mfululizo wa kwanza kati ya mifululizo miwili ya hotuba zenye kuchochea akili utakuwa na kichwa “Kumtukuza Mungu Katika Sehemu Zote za Maisha Yetu,” nao utazungumzia kwa undani maana ya maneno yaliyoongozwa kwa roho kwenye 1 Wakorintho 10:31. Mfululizo wa pili wenye kichwa, “Kutoa Utumishi Mtakatifu ili Kumsifu Yehova” utazungumzia sehemu mbalimbali za ibada yetu. Jumapili, tutakuwa na muhtasari wa Mnara wa Mlinzi na tutachunguza andiko la siku. Pia kutakuwa na fursa ya watu kubatizwa.
Wanadamu wengi hawamtambui Mungu. Wengi wanapendezwa sana na mipango ya wanadamu hivi kwamba hawatafakari kuhusu fahari ya Yehova. (Yoh. 5:44) Lakini tunasadiki kwamba kuna faida ya kutumia wakati kuchunguza jinsi ambavyo tunaweza ‘Kufanya Mambo Yote kwa Utukufu wa Mungu.’ Fanya mipango uhudhurie vipindi vyote vinne ili ufaidike kikamili.