Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/08 uku. 1
  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kulinda Jinsi Utembeavyo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kaeni Mkikesha na Kubaki Mkiwa na Akili Zenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Uandalizi kwa Ajili ya Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Uandalizi kwa Wahudumu Wakristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 8/08 uku. 1

Programu Mpya ya Kusanyiko la Mzunguko

Tunawezaje kusimama imara dhidi ya wale wanaoipinga vikali ibada ya kweli? Tunawezaje kushinda jitihada kabambe za Shetani za kutuvuta turudi katika ulimwengu usiomwogopa Mungu? Programu ya kusanyiko la mzunguko la mwaka wa utumishi wa 2009 itajibu maswali hayo muhimu. Kichwa cha kusanyiko hilo ni “Endelea Kuushinda Uovu kwa Wema.” (Rom. 12:21) Chunguza mambo tutakayojifunza.

Mwangalizi wa wilaya atatoa hotuba zifuatazo, “Tumeimarishwa Kuushinda Uovu kwa Wema,” “Jihadhari Usijiamini Kupita Kiasi!,” “Uovu Wote Utaisha Hivi Karibuni!,” na “Kuimarisha Imani Yetu Ili Kuushinda Ulimwengu.” Mwangalizi wa mzunguko atatoa hotuba zifuatazo, “Haya Ni Majira ya Kuendelea Kuwa Macho!,” inayotegemea Waroma 13:11-13, na “Usijionyeshe Kuwa Umevunjika Moyo Siku ya Taabu,” inayotegemea Methali 24:10. Tunatazamia pia hotuba ya mwangalizi wa mzunguko yenye kichwa “Mahitaji ya Mzunguko.” Hotuba nyingine yenye kuchochea itakuwa na kichwa “Je, Unaweza ‘Kuwa Katika Huduma Hii’—Kwa Kupainia?” Kutakuwa na mifululizo miwili na kichwa cha mfululizo wa kwanza ni “Simama Imara Dhidi ya Mbinu Zenye Hila za Ibilisi.” Utatusaidia kutambua na kupinga mbinu zenye hila za Ibilisi katika mambo ya kiteknolojia, burudani, na elimu. Mfululizo wenye kichwa “Jipatie Nguvu za Kumpinga Shetani Siku Hizi Zenye Uovu” utatuonyesha jinsi ya kufuata kikamili mashauri yaliyo katika Waefeso 6:10-18 ambayo yaliongozwa na roho takatifu.

Kuhubiri ujumbe wa Ufalme kunahusiana moja kwa moja na kuushinda uovu na chanzo cha uovu. (Ufu. 12:17) Haishangazi kwamba Shetani anaendelea kuwashambulia vikali Mashahidi wa Yehova! (Isa. 43:10, 12) Lakini Ibilisi atashindwa kabisa kwa sababu tumeazimia ‘kuendelea kuushinda uovu kwa wema.’ Fanya mipango kamili ili ufaidike kabisa na vipindi vyote vinne vya kusanyiko hilo la mzunguko.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki