Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Wataalamu wametambua kwamba baba ana jukumu muhimu katika maisha ya familia. Unafikiri baba mwema anapaswa kuwa na sifa gani? [Mruhusu ajibu.] Yesu alikazia jinsi mfano mzuri wa Baba yake ulivyomsaidia. [Soma Yohana 5:19.] Makala hii inazungumzia majukumu sita muhimu ya baba.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 18.
Amkeni! Okt.
“Wafuasi wa dini mbalimbali wana maoni yanayotofautiana kuhusu jinsi Mungu alivyo hasa. Lakini, Mwana wa Mungu alisema nini kuhusu jambo hilo? Ona maneno ya Yesu katika Yohana 4:24. [Soma.] Makala hii ni ya kurasa mbili peke yake, hata hivyo, inaeleza vizuri maoni ya Biblia kuhusu swali hili: “Mungu Ana Utu Gani?” Mwonyeshe makala kwenye ukurasa wa 24 na 25.
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Watu wengi hawawezi kuamini kwamba Mungu mwenye upendo anaweza kuwatesa watu milele katika moto. Unaonaje? [Mruhusu ajibu.] Biblia inafundisha wazi kwamba Mungu si mkatili wala hafurahii kuwaadhibu waovu. [Soma Ezekieli 18:23.] Nina hakika kwamba utapendezwa na maoni ya Biblia yanayozungumziwa katika gazeti hili.”
Amkeni! Nov.
“Watu wengi wana maoni ya kwamba ili mtu afanikiwe maishani lazima awe mashuhuri, tajiri, au mwenye mamlaka. Wewe una maoni gani kuhusu mafanikio? [Mruhusu ajibu.] Ona maoni ya Biblia kuhusu kinacholeta mafanikio ya kweli. [Soma Zaburi 1:1-3.] Makala hii inazungumzia njia sita za kupata mafanikio.” Mwonyeshe makala inayoanza kwenye ukurasa wa 6.