Kazi ya Kuhubiri Inatusaidia Kuendelea Kuwa Imara Kiroho
1. Kazi ya kuhubiri inatunufaishaje?
1 Tunaposhiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri, tunaweza kuimarishwa kiroho na kuwa wenye furaha zaidi. Hapana shaka kwamba sisi tunahubiri hasa ili kumpendeza Yehova. Hata hivyo, kwa kutii amri ya ‘kulihubiri neno,’ tunapata baraka za Yehova na kunufaika kwa njia nyinginezo. (2 Tim. 4:2; Isa. 48:17, 18) Kuhubiri kunaweza kutuimarishaje na kutuletea furaha?
2. Huduma yetu inatuimarishaje?
2 Tunaimarishwa na Kupata Baraka: Kuhubiri hututia moyo tukazie fikira baraka za Ufalme badala ya matatizo ya sasa. (2 Kor. 4:18) Kuwaeleza wengine mafundisho ya Biblia huimarisha imani yetu katika ahadi za Yehova na hutusaidia kuithamini zaidi ile kweli. (Isa. 65:13, 14) Tunapowasaidia wengine wakue kiroho ili ‘wasiwe sehemu ya ulimwengu,’ tunakuwa imara hata zaidi katika azimio letu la kujitenga na ulimwengu.—Yoh. 17:14, 16; Rom. 12:2.
3. Huduma inatusaidiaje kusitawisha sifa za Kikristo?
3 Kushiriki katika huduma hutusaidia kusitawisha sifa za Kikristo. Kwa mfano, kujitahidi ‘kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote,’ hutusaidia kuwa wanyenyekevu zaidi. (1 Kor. 9:19-23) Tunapozungumza na wale ambao “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji,” tunajifunza kuwa wenye huruma na hisia-mwenzi. (Mt. 9:36) Tunapostahimili licha ya ubaridi au upinzani, tunajifunza kuwa wavumilivu. Shangwe yetu inaongezeka tunapojitoa kuwasaidia wengine.—Mdo. 20:35.
4. Unahisije kuhusu huduma yako?
4 Ni baraka iliyoje kushiriki katika huduma ambayo inamletea sifa yule Mmoja ambaye anastahili ibada yetu! Huduma inatutia nguvu. Wale ambao wamejitoa kabisa “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema” wanapata baraka chungu nzima.—Mdo. 20:24.