The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy
Ni uthibitisho gani unaoonyesha kwamba Biblia ni sahihi kihistoria? Ni unabii gani mbalimbali wa Biblia uliotimizwa unaotuhakikishia kwamba yale ambayo Biblia imetabiri kuhusu wakati ujao yatatimia pia? Maswali haya yanazungumziwa katika sehemu ya tatu yenye kichwa, The Bible—Accurate History, Reliable Prophecy, iliyo katika DVD inayoitwa The Bible—A Book of Fact and Prophecy. Baada ya kutazama video hiyo, unaweza kujibu maswali yafuatayo?
(1) Ni nani aliye Chanzo cha habari zenye kutegemeka za Biblia? (Dan. 2:28) (2) Biblia inaifafanuaje Misri ya kale kwa usahihi, na unabii ulio katika Isaya 19:3, 4 ulithibitikaje kuwa wa kweli? (3) Akiolojia imethibitishaje kwamba mambo yaliyoandikwa katika Biblia kuhusu Waashuru, wafalme wao, na kuharibiwa kwa taifa lao ni ya kweli? (Nah. 3:1, 7, 13) (4) Ni unabii gani mbalimbali kuhusu Babiloni uliothibitika kuwa wenye kutegemeka? (Yer. 20:4; 50:38; 51:30) (5) Ni unabii gani uliotimia kuhusu Umedi na Uajemi? (Isa. 44:28) (6) Unabii wa Danieli 7:6 na 8:5, 8 ulitimizwaje kuhusiana na Ugiriki? (7) Andiko la Danieli 7:7 lilitimizwaje wakati Roma ilipoibuka kama serikali kuu ya ulimwengu? (8) Ni Makaisari gani wanaotajwa katika Biblia? (9) Ni nini kilichowapata Wakristo chini ya utawala wa Nero? (10) Unabii katika Ufunuo 13:11 na 17:10 ulitimizwaje? (11) Mfalme wa nane ni nani? (12) Ni sehemu gani katika video hiyo zinazothibitisha ukweli wa maneno ya Mhubiri 8:9? (13) Unangoja kwa hamu kutimizwa kwa unabii gani wakati ujao? (14) Unaweza kutumiaje video hii kuwasaidia wengine waamini kwamba Mungu ndiye Chanzo cha Biblia?