Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/11 uku. 3
  • Magazeti Yetu Yamekusudiwa Kuwavutia Watu Wengi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Magazeti Yetu Yamekusudiwa Kuwavutia Watu Wengi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Mabadiliko Yenye Kusisimua Katika Mnara wa Mlinzi!
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Toleo Jipya la Funzo la Mnara wa Mlinzi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 7/11 uku. 3

Magazeti Yetu Yamekusudiwa Kuwavutia Watu Wengi

1. Ni kwa njia gani mtumwa mwaminifu na mwenye busara anamwiga mtume Paulo?

1 Kama vile mtume Paulo alivyobadili njia aliyotumia kuhubiri habari njema ili awapate “watu wa namna zote,” mtumwa mwaminifu na mwenye busara hutumia magazeti yetu ili kuwafikia watu wa malezi na imani tofauti. (1 Kor. 9:22, 23) Ili tuyatumie vizuri magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni vizuri kuwaelewa na kuwafikiria waliokusudiwa kuyasoma.

2. Gazeti la Amkeni! limekusudiwa kuwavutia nani?

2 Amkeni!: Gazeti hili limekusudiwa kuwafikia watu walio kama wale ambao mtume Paulo aliongea nao alipohutubia “wanaume wa Athene.” (Mdo. 17:22) Wanaume hao hawakuwa na malezi ya Kikristo, na hawakuyaelewa Maandiko vizuri. Vivyo hivyo, wanaokusudiwa kusoma gazeti la Amkeni! wana ujuzi kidogo au hawana ujuzi wowote wa Biblia. Huenda hawajui lolote kuhusu mafundisho ya Kikristo, huenda wakatilia shaka dini, au labda hawajui kwamba Biblia inaweza kuwasaidia. Kusudi kuu la gazeti la Amkeni! ni kuwasadikisha wasomaji ya kuwa Mungu wa kweli yupo. Pia lengo la gazeti hilo ni kujenga imani katika Biblia na kusaidia msomaji aelewe ya kuwa Mashahidi wa Yehova ni tofauti na dini nyinginezo.

3. Toleo la watu wote na toleo la funzo la gazeti la Mnara wa Mlinzi, yanakusudiwa kusomwa na watu gani?

3 Mnara wa Mlinzi: Wanaokusudiwa kusoma toleo la watu wote la Mnara wa Mlinzi wanamheshimu Mungu na kuyaheshimu Maandiko kwa kiasi fulani. Wana ujuzi fulani wa Biblia lakini hawaelewi mafundisho yake kwa usahihi. Ni kama wale wasikilizaji ambao Paulo aliwarejezea kuwa ‘wanamwogopa Mungu.’ (Mdo. 13:14-16) Toleo la funzo la gazeti la Mnara wa Mlinzi limekusudiwa hasa Mashahidi wa Yehova. Paulo aliwaona wale waliosoma barua zake kama watu walioyajua Maandiko na waliokuwa na ujuzi sahihi kuhusu ile kweli. (1 Kor. 1:1, 2) Vivyo hivyo, makala zilizo katika toleo la funzo zimeandikwa kwa ajili ya wale wanaohudhuria mikutano na wanafahamu mafundisho na baadhi ya maneno yanayotumiwa na Mashahidi.

4. Kwa nini tusome kila toleo la magazeti tunayotumia katika utumishi wa shambani?

4 Ingawa kwa kawaida tunatoa magazeti yakiwa mawili, tunazungumzia gazeti moja tu. Kwa hiyo, jiwekee mradi wa kusoma kila toleo. Kwa kufanya hivyo, utaweza kuzungumzia makala zitakazowavutia wale unaokutana nao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki