Sanduku la Swali
◼ Je, tunapaswa kutoa sala tunapoongoza funzo la Biblia mlangoni?
Kuna faida nyingi za kuanza na kumalizia funzo la Biblia kwa sala. Tunaposali, tunamwomba Yehova atusaidie na roho yake takatifu katika mazungumzo yetu. (Luka 11:13) Pia, sala hukazia moyoni mwa mwanafunzi wetu umuhimu wa kujifunza Biblia na humfundisha jinsi ya kusali. (Luka 6:40) Kwa hiyo, ni muhimu kuanza kutoa sala haraka iwezekanavyo. Hata hivyo, kwa kuwa hali zinatofautiana, anayeongoza funzo anapaswa kutumia utambuzi ili kuamua ikiwa atatoa sala anapoongoza funzo la Biblia mlangoni.
Jambo moja muhimu tunalopaswa kufikiria ni mahali ambapo funzo linaongozewa. Ikiwa kuna kiasi fulani cha faragha, sala fupi inaweza kutolewa kwa busara, mwanzoni na mwishoni mwa funzo linaloongozwa kwa ukawaida. Lakini, ikiwa kufanya hivyo kunaweza kuvuta uangalifu usiofaa wa wapita-njia au kumfanya mwanafunzi asijihisi huru, huenda ikafaa kungoja hadi wakati ambapo funzo hilo linaweza kuongozwa mahali panapofaa zaidi. Haidhuru funzo linaongozewa wapi, tunapaswa kutumia utambuzi kuamua ni wakati gani tunapoweza kuanza kutoa sala.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 2005, ukurasa wa 4.