Mashahidi wa Yehova—Imani Yenye Matendo, Sehemu ya 1: Kutoka Gizani
Katika Biblia, nuru inahusianishwa na kweli, ilhali giza linahusianishwa na uwongo. (Zab. 43:3; Isa. 5:20) Shetani alianzisha giza duniani alipomdanganya Hawa, na hatimaye, akawaingiza wanadamu katika giza zito. (Ufu. 12:9) Video Mashahidi wa Yehova—Imani Yenye Matendo, Sehemu ya 1: Kutoka gizani inaonyesha jinsi nuru ya kiroho ilivyoanza kujitokeza kutoka gizani. (Isa. 60:1, 2) Baada ya kutazama video hiyo, je, unaweza kujibu maswali haya?
(1) Giza zito la kiroho lilieneaje baada ya kifo cha mitume? (2) Kuanzia miaka ya 1100, ni mambo gani yaliwasaidia watu kutambua kwamba makanisa yalikuwa yanafundisha uwongo? (3) Henry Grew na George Storrs walikuwa akina nani? (4) Ni matukio gani katika maisha ya Charles Russell ambayo yalibadili maisha yake? (5) Ndugu Russell, baba yake, na marafiki wengine wachache waliongoza jinsi gani darasa lao la funzo la Biblia, na ni maamuzi gani ya Kimaandiko waliyofikia? (6) Kwa nini kikundi cha Biblia cha Ndugu Russell kilijiunga na kikundi cha Nelson Barbour, hata hivyo, ni jambo gani lililosababisha Ndugu Russell ajitenge na kikundi cha Barbour? (7) Ni jambo gani lililotokea Julai 1879 ambalo lilianzisha enzi mpya ya nuru ya kiroho? (8) Baada ya hapo, Wanafunzi wa Biblia waliokuwa wakiongezeka walifanya nini ili waeneze habari njema? (9) Kwa miaka mingi kabla ya mwaka 1914, Wanafunzi wa Biblia walikuwa wakitazamia jambo gani litukie mwaka huo? (10) Wanafunzi wa Biblia walikabili hali gani ngumu baada ya kifo cha Ndugu Russell? (11) Wanafunzi wa Biblia walifanya nini baada ya Ndugu Rutherford na washiriki wenzake kuachiliwa kutoka gerezani? (12) Kutazama video hiyo kumeongezaje uthamini na uelewaji wako kuelekea tengenezo la Yehova? (13) Video hiyo imeimarishaje azimio lako la kuendelea kuhubiri kwa bidii licha ya matatizo? (14) Tunaweza kutumiaje video hiyo kuwasaidia watu wetu wa ukoo, wanafunzi wa Biblia, na wengine?
Tumeachiwa urithi wa kiroho wenye thamani kama nini na Wanafunzi hao wa Biblia wa mapema! Walikuwa wamulikaji wa nuru wenye bidii na ujasiri katika ulimwengu ulio katika giza la kiroho. Acheni tuige mfano wao na ‘tuendelee kutembea kama watoto wa nuru.’—Efe. 5:8.