Mashahidi wa Yehova—Imani Yenye Matendo, Sehemu ya 2: Nuru na Iangaze
Baada ya Ndugu Rutherford na wenzake kuachiliwa kutoka gerezani mnamo 1919, Wanafunzi wa Biblia walikuwa na kazi kubwa sana ya kufanya. Kama inavyoonyeshwa katika video Mashahidi wa Yehova—Imani Yenye Matendo, Sehemu ya 2: Nuru na Iangaze, Wanafunzi wa Biblia wangekuwa na wapinzani wengi, uelewaji wao wa Maandiko ungeendelea kuongezeka, na imani yao ingeboreshwa. (Met. 4:18; Mal. 3:1-3; Yoh. 15:20) Baada ya kutazama video hiyo, je, unaweza kujibu maswali haya?
(1) Wanafunzi wa Biblia walitumia njia gani mbalimbali ili kueneza habari njema? (2) Ni nini kilichotangazwa wakati wa makusanyiko yaliyokuwa ya pekee sana ya mwaka wa 1931 na 1935? (3) Ni habari gani muhimu iliyozungumziwa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Novemba 1, 1939? (4) Eleza kile kilichotukia katika jumba la Madison Square Garden wakati Ndugu Rutherford alipokuwa akitoa hotuba yenye kichwa “Serikali na Amani.” (5) Ni nini kilichovutia sana katika hotuba ya Ndugu Knorr yenye kichwa “Amani—Je, Inaweza Kudumu?” (6) Mnamo 1942, Mashahidi wa Yehova walifanya mipango gani ili kupanua kazi yao ya kuhubiri? (7) Eleza baadhi ya mapambano ya kisheria yaliyofanyika Marekani, Kanada, na Ugiriki. (8) Shule ya Gileadi ilikuwa na matokeo gani katika ukuzi wa kazi ya kuhubiri? (9) Ni kazi gani muhimu iliyoanzishwa mwaka wa 1946, na kwa nini? (10) Mashahidi wa Yehova walichukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba mwenendo wao unapatana na viwango vya Biblia? (11) Eleza baadhi ya marekebisho yaliyofanywa miaka ya 1970 ili kupatanisha tengenezo na kielelezo kilicho katika Biblia. (12) Kutazama video hiyo kumekusaidiaje kuelewa zaidi kwamba Yehova anaongoza mambo na kuwa hili ni tengenezo lake? (13) Video hiyo imeimarishaje azimio lako la kuendelea kuhubiri kwa bidii licha ya vipingamizi? (14) Tunaweza kuitumiaje video hiyo kuwasaidia watu wetu wa ukoo, wanafunzi wa Biblia, na wengine?
Kila siku, kuna mambo mapya yanayotukia ambayo huchangia katika Historia ya Mashahidi wa Yehova. Historia itaonyesha nini kuhusiana na jitihada zetu katika huduma? Kama walivyofanya ndugu zetu, acheni tuendelee kwa bidii kuacha ‘nuru iangaze’!—2 Kor. 4:6.