Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/12 uku. 1
  • Sababu 12 za Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu 12 za Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Thamini Pendeleo Lako la Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Huduma Yetu Inaonyesha Kwamba Tunampenda Mungu
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Kuendeleza Huduma Yetu Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Dumisha Bidii Yako Katika Huduma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 6/12 uku. 1

Sababu 12 za Kuhubiri

Kwa nini sisi huhubiri na kuongoza mafunzo ya Biblia? Je, sababu ya msingi ni kuwasaidia watu wenye mioyo minyoofu waingie katika barabara inayoongoza kwenye uzima? (Mt. 7:14) Hiyo ndiyo sababu ya kwanza iliyoorodheshwa hapa chini, lakini si sababu kuu. Kati ya sababu 12 zifuatazo za kuhubiri, unafikiri ni ipi iliyo muhimu zaidi?

1. Kuhubiri husaidia kuokoa uhai.​—Yoh. 17:3.

2. Husaidia kuonya waovu.​—Eze. 3:18, 19.

3. Huchangia kutimia kwa unabii wa Biblia.​—Mt. 24:14.

4. Huonyesha uadilifu wa Mungu. Hakuna mtu anayeweza kudai kwamba Yehova aliangamiza waovu bila kuwapa nafasi ya kutubu.​—Mdo. 17:30, 31; 1 Tim. 2:3, 4.

5. Hutuwezesha kutimiza wajibu wetu wa kuandaa msaada wa kiroho kwa watu walionunuliwa kwa damu ya Yesu.​—Rom. 1:14, 15.

6. Hutusaidia kuepuka hatia ya damu.​—Mdo. 20:26, 27.

7. Ni takwa ili sisi wenyewe tuokolewe.​—Eze. 3:19; Rom. 10:9, 10.

8. Huonyesha upendo kwa jirani.​—Mt. 22:39.

9. Huonyesha utii wetu kwa Yehova na kwa Mwana wake.​—Mt. 28:19, 20.

10. Ni sehemu ya ibada yetu.​—Ebr. 13:15.

11. Huonyesha kwamba tunampenda Mungu​.—1 Yoh. 5:3.

12. Huchangia kulitakasa jina la Yehova.​—Isa. 43:10-12; Mt. 6:9.

Bila shaka, kuna sababu nyingine zaidi za kuhubiri. Kwa mfano, kuhubiri huimarisha imani yetu na pia tunapata pendeleo la kuwa wafanyakazi wenzi wa Mungu. (1 Kor. 3:9) Hata hivyo, sababu muhimu zaidi ya kuhubiri ni namba 12. Hata itikio liweje, kuhubiri huchangia kulitakasa jina la Mungu ili Yehova amjibu yule anayemdhihaki. (Met. 27:11) Kwa kweli, tuna sababu nzuri sana za ‘kuendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema.’​—Mdo. 5:42.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki