Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/13 uku. 2
  • Ni Nani Watakaopendezwa na Makala Hii?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Watakaopendezwa na Makala Hii?
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Weka Kando Wakati kwa Ajili ya Utendaji wa Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Teua Makala za Kuvutia Mapendezi Hususa ya Watu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 5/13 uku. 2

Ni Nani Watakaopendezwa na Makala Hii?

1. Tunaposoma magazeti yetu ya Mnara wa Mlinzi au Amkeni! tunapaswa kuzingatia nini, na kwa nini?

1 Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yameandaliwa kwa ajili ya watu ulimwenguni pote. Kwa hiyo, makala za magazeti hayo zinazungumzia mambo mbalimbali. Tunaposoma kila makala katika magazeti yetu ya kibinafsi, tunapaswa kufikiria ni nani hasa anayeweza kupendezwa na makala hizo, na kisha tufanye mipango ya jinsi ya kumwachia mtu huyo magazeti hayo.

2. Ni habari gani zinazozungumziwa katika magazeti yetu zinazoweza hasa kuwavutia watu?

2 Je, gazeti la karibuni la Mnara wa Mlinzi linazungumzia habari fulani ya Biblia ambayo wewe na mfanyakazi mwenzako mlizungumzia awali? Je, kuna makala inayohusu maisha ya familia inayoweza kumsaidia mtu wa ukoo? Je, kuna mtu unayefahamiana naye anayepanga kusafiri katika nchi ambayo imezungumziwa kwenye Amkeni!? Je, kuna gazeti linaloweza kuwavutia wafanyabiashara fulani au mashirika ya serikali katika eneo lenu? Kwa mfano, gazeti linalozungumzia matatizo yanayowakabili wazee huenda likafaa hasa katika makao ya kuwatunzia wazee. Maafisa wa kutekeleza sheria wanaweza kuvutiwa na gazeti linalozungumzia uhalifu.

3. Simulia jambo lililoonwa linaloonyesha umuhimu wa kutoa magazeti hususa kwa wale tunaohisi kwamba wanaweza kupendezwa na magazeti hayo.

3 Matokeo: Baada ya kupokea gazeti la Amkeni! la Oktoba 2011 lenye kichwa “Kuwalea Watoto Wenye Kutegemeka,” wenzi wa ndoa kutoka Afrika Kusini walipiga simu kwenye shule 25 zilizo katika eneo la kutaniko lao. Shule ishirini na mbili zilikubali magazeti hayo na kuyasambaza kwa wanafunzi. Wenzi wengine katika nchi hiyo walikuwa na wazo kama hilo nao waliyatoa magazeti hayo katika shule zilizo kwenye eneo lao. Walimu katika mojawapo ya shule hizo waliamua kutumia magazeti hayo katika vipindi vya masomo. Wenzi hao walimsimulia mwangalizi wa mzunguko mambo waliyojionea. Kisha mwangalizi huyo akayatia moyo makutaniko katika mzunguko wake yatembelee shule zilizo katika eneo lao. Ofisi ya tawi ilipokea maombi mengi sana ya magazeti zaidi hivi kwamba gazeti hilo likachapishwa tena!

4. Kwa nini tunataka kuwapa magazeti watu wengi iwezekanavyo?

4 Magazeti yetu yanazungumzia maana halisi ya matukio ya sasa na yanaelekeza uangalifu kwenye Biblia na Ufalme wa Mungu. Hayo ndio magazeti pekee duniani ‘yanayotangaza wokovu.’ (Isa. 52:7) Kwa hiyo, tungependa kuwapa watu wengi iwezekanavyo magazeti hayo. Njia nzuri ya kufanya hivyo ni kujiuliza, ‘Ni nani watakaopendezwa na makala hii?’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki