Tumia Video Unapofundisha
Yehova alipowasilisha habari muhimu kwa Abrahamu na Yeremia, alifanya hivyo si kwa kuwaambia tu bali pia kwa kuwaonyesha habari hizo. (Mwa. 15:5; Yer. 18: 1-6) Tunaweza kuwasaidia wanafunzi wetu waelewe na wathamini kweli za Biblia kwa kutumia video zetu vizuri. Yafuatayo ni mapendekezo kuhusu wakati tunaoweza kutumia baadhi ya video zetu. Kumbuka kwamba hayo ni mapendekezo tu kwani kila mwanafunzi ni tofauti.
Kitabu Biblia Inafundisha
◻ Sura ya 1: Baada ya fungu la 17, tazameni Maajabu ya Uumbaji Yanafunua Utukufu wa Mungu
◻ Sura ya 2: Mwishoni mwa sura, tazameni The Bible—Mankind’s Oldest Modern Book
◻ Sura ya 9: Baada ya fungu la 14, tazameni Jehovah’s Witnesses—Organized to Share the Good News
◻ Sura ya 14: Mwishoni mwa sura, tazameni The Bible—Its Power in Your Life
◻ Sura ya 15: Baada ya fungu la 10, tazameni Our Whole Association of Brothers
Kitabu “Upendo wa Mungu”
◻ Sura ya 3: Baada ya fungu la 15, tazameni Young People Ask—How Can I Make Real Friends?
◻ Sura ya 4: Mwishoni mwa sura, tazameni Heshimu Mamlaka ya Yehova
◻ Sura ya 7: Baada ya fungu la 12, tazameni No Blood—Medicine Meets the Challenge
◻ Sura ya 9: Baada ya fungu la 6, tazameni Vielelezo vya Kuonya Leo
◻ Sura ya 17: Mwishoni mwa sura, tazameni ‘Tembea kwa Imani Si kwa Kuona’
Je, mwanafunzi wako wa Biblia anaweza kunufaika kwa kutazama video nyinginezo? Kwa mfano, wanafunzi wanaokabili upinzani wanaweza kutiwa moyo kwa kutazama video Waaminifu Chini ya Majaribu—Mashahidi wa Yehova Katika Muungano wa Sovieti au Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault. Vijana wanaweza kufaidika kwa kutazama video Pursue Goals That Honor God na Vijana Huuliza—Nitayatumiaje Maisha Yangu? Weka alama kwenye kitabu Biblia Inafundisha na “Upendo wa Mungu” ili ukumbuke wakati utakapotazama video na mwanafunzi wako au utakapomwazima aitazame. Kadiri video mpya zinavyotolewa fikiria jinsi unavyoweza kuzitumia kugusa mioyo ya wanafunzi wako wa Biblia.—Luka 24:32.