Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/13 uku. 1
  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Yoeli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Yoeli
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 29—Yoeli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kuvumilia Majaribu Kulitusaidia Kumtegemea Yehova Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Yoeli Atoa Unabii juu ya Kisasi cha Yehova na Upendo Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Shambulizi Kutoka Kaskazini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 7/13 uku. 1

Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Yoeli

1. Tunawezaje kuiga unyenyekevu wa Yoeli tunapohubiri?

1 Nabii Yoeli alikuwa nani? Anajitambulisha tu kwamba alikuwa “mwana wa Pethueli.” (Yoe. 1:1) Nabii huyo mnyenyekevu alikazia ujumbe wa Yehova na si jukumu lake mwenyewe akiwa mjumbe. Vivyo hivyo tunaposhiriki katika huduma yetu, badala ya kujitafutia sifa au umaarufu, tunaelekeza fikira za watu kwa Yehova na kwenye Biblia. (1 Kor. 9:16; 2 Kor. 3:5) Kwa kuongezea, ujumbe tunaotangaza hutuimarisha. Ni mambo gani yaliyo katika unabii wa Yoeli yanayoweza kutuchochea tuwe na tumaini na wenye bidii leo?

2. Kukaribia kwa siku ya Yehova kunapaswa kutuchochea tufanye nini?

2 “Siku ya Yehova Iko Karibu.” (Yoe. 1:15): Ingawa maneno hayo yaliandikwa maelfu ya miaka iliyopita, tunaishi katika kipindi cha mwisho cha utimizo wa maneno hayo. Hali za ulimwengu zinazozorota na upinzani na dhihaka ambazo tunakabili katika eneo letu ni uthibitisho ulio wazi kwamba tunaishi katika siku za mwisho za mfumo huu wa mambo. (2 Tim. 3:1-5; 2 Pet. 3:3, 4) Tunapofikiria kuhusu jinsi mwisho ulivyo karibu tuna kila sababu ya kutanguliza huduma maishani mwetu.​—2 Pet. 3:11, 12.

3. Kwa nini huduma yetu ni muhimu sana hasa tunapokaribia dhiki kuu?

3 “Yehova Atakuwa Kimbilio kwa Watu Wake.” (Yoe. 3:16): Neno kutikiswa katika mstari huu linaweza tu kurejelea hukumu ya Yehova itakayotekelezwa katika dhiki kuu. Tunafarijiwa kujua kwamba Yehova atawakomboa watumishi wake waaminifu wakati huo. (Ufu. 7:9, 14) Tunapofanya kazi ya kuhubiri na kuona jinsi Yehova anavyotutegemeza na kutuimarisha, tunajenga imani yetu na uvumilivu utakaotusaidia katika dhiki kuu inayokuja.

4. Kwa nini tunaweza kuwa wenye shangwe na kutazamia wakati ujao tukiwa na uhakika?

4 Ingawa wengine husema kwamba ujumbe wa Yoeli unahuzunisha, ujumbe huo huwapa watu wa Mungu tumaini zuri ajabu la kukombolewa. (Yoe. 2:32) Basi na tutazamie wakati ujao tukiwa na uhakika na kutangaza kwa bidii habari njema ya Ufalme wa Mungu huku tukitii maneno ya Yoeli 2:23: “Furahini na mshangilie katika Yehova Mungu wenu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki