Sanduku La Swali
◼ Je, dada anapaswa kufunika kichwa anapoongoza funzo la Biblia mlangoni akiwa na mhubiri mwanamume?
Dada anapoongoza funzo rasmi la Biblia, na ameambatana na ndugu, anapaswa afunike kichwa. (1 Kor. 11:3-10) Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Julai 15, 2002, ukurasa wa 27, linaeleza hivi: “Kwa kuwa funzo hilo huwa limepangwa kimbele, mwenye kuongoza anafundisha na kusimamia. Chini ya hali hizi, funzo hilo ni kama mkutano wa ziada. Dada akiongoza funzo hilo akiwa pamoja na ndugu aliyebatizwa, anapaswa kufunga kitambaa kichwani.” Inapaswa kuwa hivyo iwe funzo linaongozwa nyumbani, mlangoni, au mahali pengine popote.
Kwa upande mwingine, ikiwa funzo rasmi halijaanzishwa, dada hatahitaji kufunika kichwa akiwa ameandamana na ndugu, hata kama kusudi la ziara ya kurudia ni kuonyesha jinsi funzo la Biblia hufanywa au kuzungumzia habari ambayo inapatikana katika mojawapo ya machapisho yaliyokusudiwa kuwafundisha watu Biblia. Kwa sababu funzo la Biblia mlangoni huanzishwa hatua kwa hatua kupitia ziara kadhaa za kurudia, wahubiri watahitaji kufikiria hali na kutumia utambuzi ili kuamua ni wakati gani utakaofaa kuanza kufunika kichwa.