Tumia Magazeti ya Zamani Vizuri
Kwa sababu magazeti ya zamani hayamnufaishi mtu yeyote ikiwa yanatupwa au kuhifadhiwa, tunapaswa kuwapa wanaopendezwa. Gazeti moja tu linaweza kumchochea mtu apendezwe na kweli na aanze kuliitia jina la Yehova. (Rom. 10:13, 14) Yafuatayo ni mapendekezo ya jinsi ya kuyatumia vizuri magazeti ya zamani.
Unapohubiri katika maeneo ambayo hayahubiriwi kwa ukawaida, unaweza kuacha kwenye nyumba ambazo hukupata watu.
Unapohubiri katika maeneo ya umma kama vile kwenye vituo vya mabasi au vya treni, waulize ikiwa wangependa kusoma chapisho fulani, kisha waonyeshe magazeti kadhaa ya zamani uliyonayo, na uwape nafasi ya kuchagua.
Unapotembelea hospitali, ofisi za umma, au sehemu kama hizo katika eneo la kutaniko lenu, acha nakala chache za magazeti ya zamani ili watu wanaosubiri huduma wayasome. Itafaa ikiwa kwanza utaomba kibali kutoka kwa msimamizi wa sehemu hiyo iwapo anapatikana. Ukiona tayari kuna nakala za magazeti yetu, usiache mengine.
Unapojitayarisha kufanya marudio, fikiria mapendezi ya kila mtu unayepanga kumtembelea. Je, ana familia? Anapenda kusafiri? Kutunza bustani? Pitia magazeti ya zamani ili uone ikiwa kuna makala ambayo huenda akafurahia kusoma, halafu umwonyeshe makala hiyo unapomtembelea tena.
Ukimpata tena mtu anayependezwa baada ya kumkosa mara kadhaa, mwonyeshe nakala za zamani ambazo bado hajapata.