KICHWA CHA MWEZI HUU: “Lihubiri neno, fanya hivyo kwa bidii.”—2 Tim. 4:2.
Kueleza Mambo Tunayoamini Kuhusu Mwaka wa 1914
Maandiko yanatutia moyo ‘tuwe tayari kutetea’ mambo tunayoamini, ‘tukifanya hivyo kwa tabia-pole na heshima kubwa.’ (1 Pet. 3:15) Kwa kweli, inaweza kuwa vigumu kufafanua kweli zenye kina za Biblia, kama vile jinsi tunavyojua kwamba Ufalme ulianza kutawala mwaka wa 1914. Makala zenye kichwa “Mazungumzo Pamoja na Jirani—Ufalme wa Mungu Ulianza Kutawala Lini?” zimetayarishwa ili zitusaidie. Makala hizo zinapatikana katika magazeti ya Mnara wa Mlinzi ambayo tutatoa katika huduma mwezi wa Oktoba na Novemba. Unapochunguza makala hizo, fikiria maswali yafuatayo kuhusu njia ambayo Cameron alitumia.
Ni kwa njia gani . . .
alitumia pongezi ili kuweka msingi mzuri wa mazungumzo kuhusu mambo wanayokubaliana?—Mdo. 17:22.
alieleza mambo anayoamini kwa unyenyekevu?—Mdo. 14:15.
Kwa nini ilifaa kwamba . . .
alirudia mambo ambayo ametoka kuzungumzia kabla ya kuendelea na mazungumzo?
alitua mara kwa mara na kumuuliza mwenye nyumba ikiwa ameelewa mambo ambayo tayari ameyazungumzia?
hakuzungumzia mambo mengi sana kwa wakati mmoja? —Yoh. 16:12.
Tunamshukuru sana Yehova, ‘Mfundishaji wetu Mkuu,’ kwa kutufundisha jinsi ya kufafanua kweli zenye kina za Biblia kwa watu wenye njaa ya kiroho!—Isa. 30:20.