Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Aprili 1
“Leo tunampa kila mtu katika eneo lenu trakti hii. [Mpatie trakti Una maoni gani kuhusu Biblia? kisha muulize swali lililo katika ukurasa wa kwanza. Mwonyeshe jibu la Biblia katika 2 Timotheo 3:16, na umtie moyo aisome trakti hiyo.] Watu wengi hawajui kwamba Biblia ina majibu yenye kuridhisha kwa maswali haya. [Mwonyeshe swali lililo katika ukurasa wa mbele wa gazeti la Mnara wa Mlinzi.] Gazeti hili linaeleza jinsi unavyoweza kupata majibu katika Biblia yako.”
Amkeni Aprili
“Tumewatembelea kwa ufupi leo, kwa sababu watu wengi huhangaikia mabadiliko wanayoyaona katika familia zao. Miaka iliyopita, wazazi walikuwa na mamlaka, lakini sasa katika familia fulani inaonekana kwamba watoto ndiyo wenye mamlaka. Je, unafikiri leo wazazi wanawatia nidhamu au adabu watoto wao katika njia inayofaa? [Mruhusu ajibu.] Kulingana na Biblia, nidhamu ni muhimu. [Soma Methali 29:17.] Gazeti hili linazungumzia maagizo ya Biblia yenye usawaziko kuhusu kuwatia nidhamu watoto.”