Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Kuwazoeza Wapya
Kwa Nini Ni Muhimu: Wanafunzi wapya wa Yesu wanapaswa kushika “mambo yote” ambayo aliamuru, na hilo linatia ndani kuwafundisha wengine kweli. (Mt. 28:19, 20) Wanafunzi wengi wapya tayari wamestahili kujiunga na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na huenda wamewahubiria isivyo rasmi marafiki au watu wao wa ukoo. Hata hivyo, wanapoendelea kuthamini zaidi mambo wanayojifunza na kujua kwamba Yehova anataka watu wote wasikie habari njema, huenda wakaonyesha tamaa yao ya kushiriki katika huduma ya shambani. (Rom. 10:13, 14) Wanafunzi wanapostahili kuwa wahubiri ambao hawajabatizwa, wanahitaji kuzoezwa vizuri ili wawe na ujasiri zaidi katika hatua hii muhimu ya maendeleo yao ya kiroho.—Luka 6:40.
Jaribu Kutumia Dokezo Hili kwa Mwezi Mzima:
Ikiwa unajifunza na mwanafunzi ambaye amekuwa mhubiri, mwalike ahubiri nawe katika utumishi wa nyumba kwa nyumba, na uandamane naye unapofanya ziara ya kurudia au unapoongoza funzo la Biblia. Ikiwa hujifunzi na mhubiri mpya, mwalike mhubiri ambaye hana uzoefu sana katika huduma, ahubiri pamoja nawe.