Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/15 uku. 2
  • “Maneno Haya . . . Lazima Yawe Moyoni Mwako”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Maneno Haya . . . Lazima Yawe Moyoni Mwako”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha​—Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ibada ya Familia​—Je, Mnaweza Kuifanya Ifurahishe Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Isaidie Familia Yako Kumkumbuka Yehova
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 8/15 uku. 2

“Maneno Haya . . . Lazima Yawe Moyoni Mwako”

Wazazi ni kama wachungaji. Ni lazima wawatunze vizuri watoto wao, kwa kuwa watoto wanaweza kukengeushwa na kushambuliwa kwa urahisi. (Met. 27:23) Wazazi wanawezaje kutimiza daraka hilo? Lazima kila siku watumie wakati kuwasiliana na watoto wao ili kujua yale yaliyo akilini na moyoni mwao. (Met. 20:5) Pia, wazazi wanapaswa kujenga kwa vifaa visivyoweza kushika moto ili waimarishe imani ya watoto wao. (1 Kor. 3:10-15) Kwa kuwa ibada ya familia inayoongozwa kwa ukawaida ni muhimu sana ili kutimiza lengo hilo, tazameni video “Maneno Haya . . . Lazima Yawe Moyoni Mwako” mkiwa pamoja katika familia yenu, kisha mzungumzie maswali yafuatayo.

(1) Ni nini kilichofanya familia ya Mrema iache kutanguliza mambo ya kiroho? (2) Kwa nini mwanzoni Ndugu Mrema hakufanikiwa alipojaribu kuongoza ibada ya familia? (3) Ni njia gani ya Kimaandiko inayoweza kuwasaidia wazazi kupata matokeo bora wanapowalea watoto wao? (Kum. 6:6, 7) (4) Ni nini kinachoweza kusaidia familia kuwa na mawasiliano mazuri zaidi? (5) Watoto wanahitaji wazazi wajidhabihu katika njia gani? (6) Ndugu na Dada Baraza walikuwa mfano mzuri kwa familia ya Mrema katika njia gani? (Met. 27:17) (7) Kichwa cha familia anapaswa kufanya nini mapema ili ibada ya familia ifanikiwe? (8) Ndugu Mrema alianza kufanya nini ili kuboresha hali katika familia yake? (9) Kwa nini ni muhimu kufanya ibada ya familia kwa ukawaida? (Efe. 6:4) (10) Ni mambo gani yanayoweza kufanywa katika ibada ya familia? (11) Ni katika njia gani Ndugu Mrema alikuwa mtulivu lakini thabiti alipokuwa akimsaidia Marko kuona umuhimu wa kufanya yaliyo sawa? (Yer. 17:9) (12) Ndugu na Dada Mrema walimsaidiaje Rebeka kufanya uamuzi unaofaa kuhusu uhusiano wake na Justin? (Marko 12:30; 2 Tim. 2:22) (13) Ndugu na Dada Mrema walionyeshaje imani walipokuwa wakifanya mabadiliko katika maisha yao? (Mt. 6:33) (14) Video hii inakaziaje daraka la vichwa vya familia la kuandaa mahitaji ya kiroho ya familia zao? (1 Tim. 5:8) (15) Ukiwa kichwa cha familia, umeazimia kufanya nini?

TAARIFA KWA VICHWA VYA FAMILIA: Drama hii ya kisasa iliigizwa katika programu ya kusanyiko la eneo la mwaka wa 2011. Wakati huo, je, ulitambua mambo fulani kuhusu ibada yenu ya familia uliyohitaji kufanyia kazi? Namna gani wakati huu? Ikiwa bado kuna mambo unayohitaji kuboresha, tafadhali sali kwa Yehova akusaidie kufanya mabadiliko hayo ili familia yako ifaidike milele.—Efe. 5:15-17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki