Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
“Je, umewahi kujiuliza Mashahidi wa Yehova walipata wapi jina lao? [Mruhusu ajibu.] Jibu linapatikana katika Biblia, ambapo Mungu amefunua jina lake la kibinafsi. [Soma Zaburi 83:18.] Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunatangaza habari njema kumhusu yeye na kusudi lake kwa wanadamu. Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linarekebisha maoni yasiyo ya kweli kutuhusu.”
Amkeni! Septemba
“Watu wengi wanakubali kwamba tunahitaji pesa ili tuishi. Lakini unafikiri kuna hatari kuhangaikia pesa kupita kiasi? [Mruhusu ajibu.] Ona onyo ambalo Biblia inatoa. [Soma 1 Timotheo 6:9.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa.”