HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 34-37
Mtegemee Yehova na Ufanye Mema
“Usiwaonee wivu wale wanaofanya mambo yasiyo ya uadilifu”
Usiruhusu mafanikio ya muda mfupi ya watu waovu yakukengeushe na kukufanya uache kumtumikia Yehova. Kazia fikira baraka na miradi ya kiroho
“Mtegemee Yehova na ufanye mema”
Uwe na hakika kwamba Yehova atakutegemeza unapokuwa na shaka au mahangaiko. Atakusaidia uendelee kuwa mwaminifu
Uwe na bidii katika kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu
‘Pata furaha tele katika Yehova’
Tenga wakati wa kusoma na kutafakari Neno la Mungu ukiwa na lengo la kumjua Yehova vizuri zaidi
“Mkabidhi Yehova njia yako”
Uwe na uhakika kabisa kwamba Yehova atakusaidia kukabiliana na tatizo lolote
Dumisha mwenendo mzuri unapokabili upinzani, mateso, au watu wanaposema uwongo kukuhusu
“Kaa kimya mbele za Yehova na kumngojea kwa kutamani”
Epuka kutenda haraka-haraka kwa njia inayoweza kukunyang’anya shangwe na usalama wa kiroho
“Wapole wataimiliki dunia”
Tafuta upole, na umngojee Yehova kwa unyenyekevu hadi atakapoondoa ukosefu wote wa haki unaokabili
Wategemeze waabudu wenzako na kuwafariji walioshuka moyo kwa kuwaeleza ahadi ya ulimwengu mpya wa Mungu, ambayo itatimia hivi karibuni
Ufalme wa Kimasihi utaleta baraka nyingi