HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ZABURI 102-105
Yehova Anakumbuka Sisi Ni Mavumbi
Daudi alitumia usemi wa mfano kukazia rehema za Yehova.
Kama tu ambavyo ni vigumu kwetu kuelewa kihalisi umbali uliopo kati ya dunia na mbingu zenye nyota, vivyo hivyo pia hatuwezi kuelewa kikamili wingi wa upendo mshikamanifu wa Yehova
Yehova anaweka makosa yetu mbali sana nasi kwa kadiri tusiyoweza kuwazia, kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi
Kama vile baba anavyomwonyesha rehema mwana wake aliyeumia, ndivyo Yehova anavyowaonyesha rehema wale ambao wametubu na kuhuzunishwa sana na dhambi zao