HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ISAYA 29-33
“Mfalme Atatawala kwa Ajili ya Uadilifu”
Yesu, Mfalme anayetawala, anatupatia “wakuu” au wazee wa kutunza kundi
Kama “mahali pa kujificha kutokana na dhoruba ya mvua,” wanafanya kazi ya kulinda kundi kutokana na dhoruba ya mateso na kuvunjika moyo
Kama “vijito vya maji katika nchi isiyo na maji,” wanawaburudisha wale wenye kiu ya kiroho kwa kuwapatia kweli safi na isiyochanganywa na kitu
Kama “kivuli cha mwamba mzito katika nchi iliyochoka,” wanalipatia kundi kitulizo kwa kutoa miongozo na burudisho la kiroho