Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Juni uku. 7
  • Dumisha Viwango vya Yehova vya Maadili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dumisha Viwango vya Yehova vya Maadili
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Viwango vya Yehova Vinatusaidia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Juni uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Dumisha Viwango vya Yehova vya Maadili

Yehova Mungu ndiye anayewawekea wanadamu kiwango cha maadili. Kwa mfano, ameweka sheria kwamba ndoa ni muungano wa kudumu kati ya mwanamume na mwanamke. (Mt 19:4-6, 9) Anashutumu aina zote za uasherati. (1Ko 6:9, 10) Hata anatoa kanuni kuhusiana na mavazi na mapambo yanayowafanya watu wake wawe tofauti na watu wengine.—Kum 22:5; 1Ti 2:9, 10.

Katika ulimwengu wa leo, watu wengi wanakataa viwango vya Yehova. (Ro 1:18-32) Wanaruhusu maoni ya wengi yaathiri jinsi wanavyovaa, kujipamba, na kujiendesha. Wengi wanatukuza mwenendo wao uliopotoka kupindukia na kuwachambua wale wanaoishi kwa njia tofauti.—1Pe 4:3, 4.

Tukiwa Mashahidi wa Yehova, lazima tudumishe viwango vya Mungu vya maadili kwa ujasiri. (Ro 12:9) Jinsi gani? Kwa busara, tunapaswa kuwajulisha watu kile kinachokubalika kwa Mungu. Lakini sisi pia tunahitaji kudumisha viwango vya juu katika maisha yetu wenyewe. Kwa mfano, tunapochagua mitindo ya mavazi na kujipamba, huenda ikafaa kujiuliza: ‘Je, uchaguzi wangu unaonyesha viwango vya Yehova au vya ulimwengu? Je, mavazi na mapambo yangu yananitambulisha kuwa Mkristo anayemwogopa Mungu?’ Au ninapochagua kipindi au sinema ya kutazama, huenda ikafaa kujiuliza: ‘Je, Yehova anaona kuwa kipindi hiki kinafaa? Kinaonyesha viwango vya nani vya maadili? Je, burudani ninazochagua zinaweza kudhoofisha ulinzi wangu wa maadili?’ (Zb 101:3) Je, kinaweza kuwakwaza washiriki wa familia yangu au watu wengine?’—1Ko 10:31-33.

Kwa nini ni muhimu sana kwetu kudumisha viwango vya Yehova vya maadili? Kristo Yesu ataharibu mataifa hivi karibuni na kuondoa uovu wote. (Eze 9:4-7) Ni wale tu wanaofanya mapenzi ya Mungu watakaobaki. (1Yo 2:15-17) Acheni sisi tutetee viwango vya Yehova vya maadili ili watu wote wanaoshuhudia mwenendo wetu mzuri wamtukuze Mungu.—1Pe 2:11, 12.

Mwanamke akichagua mavazi

Uchaguzi wangu wa mavazi na mapambo unafunua nini kuhusu viwango vyangu vya maadili?

TAZAMENI VIDEO UWE RAFIKI YA YEHOVA—MWANAMUME MMOJA, MWANAMKE MMOJA, KISHA MZUNGUMZIE MASWALI YAFUATAYO:

  • Kwa nini ni jambo la hekima kuishi kupatana na viwango vya Yehova?

  • Kwa nini wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao viwango vya maadili vya Yehova wanapokuwa wachanga?

  • Vijana na wazee wanaweza kuwasaidiaje watu wanufaike kutokana na wema wa Mungu?

UNAWEZA KUSEMA NINI MTU AKISEMA . . .

  • “Una maoni gani kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja?”

  • “Maoni ya Biblia kuhusu ngono kati ya watu wa jinsia moja yamepitwa na wakati!”

  • “Watu wanaofanya ngono na watu wa jinsia yao hawawezi kubadilika; walizaliwa hivyo.”

(yp1 sura ya 23; yp2 sura ya 28)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki