MAISHA YA MKRISTO
Wazoeze Kumtumikia Yehova Daima
Mambo yaliyoonwa yanaonyesha kwamba wahubiri wapya wanaozoezwa tangu mwanzo kushiriki katika huduma kwa bidii na kwa ukawaida, mara nyingi wanakuwa wahubiri wenye matokeo. (Met 22:6; Flp 3:16) Yafuatayo ni mapendekezo ya jinsi ya kumsaidia mwanafunzi kujiwekea msingi mzuri kwa ajili ya huduma:
Mara tu mwanafunzi wako anapostahili kuwa mhubiri, anza kumzoeza. (km 8/15 1) Kazia ndani yake umuhimu wa kuhakikisha kwamba kuhubiri ni sehemu ya ratiba yake ya kila juma. (Flp 1:10) Zungumza kwa njia inayofaa kuhusu eneo lenu. (Flp 4:8) Mtie moyo ahubiri pamoja na mwangalizi wa kikundi na wahubiri wengine ili afaidike kutokana na uzoefu wao.—Met 1:5; km 10/12 6 ¶3
Mwanafunzi anapobatizwa, usiache kumtia moyo na kumzoeza katika huduma, hasa ikiwa hajamaliza kujifunza kitabu “Upendo wa Mungu.”—km 12/13 7
Tumia utangulizi rahisi unapohubiri pamoja na mhubiri mpya. Baada ya kusikiliza jinsi anavyohubiri, mpongeze sana. Mpe mapendekezo yatakayomsaidia awe na matokeo zaidi.—km 5/10 7