HAZINA ZA NENO LA MUNGU | NAHUMU 1–HABAKUKI 3
Endelea Kuwa Macho Kiroho na Mwenye Bidii
Huenda haikuonekana kama Wababiloni wangeweza kuiharibu Yuda. Taifa la Yuda lilikuwa chini ya uvutano wenye nguvu wa Misri na haikuonekana kama Wakaldayo walikuwa na nguvu kuliko Misri. Isitoshe, kwa Wayahudi wengi, lilikuwa jambo lisiloweza kuwaziwa kwamba Yehova angeruhusu Yerusalemu na hekalu lake kuharibiwa. Hata hivyo, unabii ungetimia na Habakuki alihitaji kuutarajia kwa kuendelea kuwa macho kiroho na mwenye bidii.
Ni nini kinachonihakikishia kwamba mwisho wa mfumo huu wa mambo uko karibu sana?
Ninaweza kufanya nini ili niendelee kuwa macho kiroho na mwenye bidii?