MAISHA YA MKRISTO
Endelea Kuwa Macho Kiroho na Mwenye Bidii Hali Zinapobadilika
Mabadiliko hayaepukiki, hasa katika siku hizi za mwisho. (1Ko 7:31) Iwe ni mabadiliko tuliyotarajia au la, iwe ni mazuri au mabaya, yanaweza kuvuruga ibada yetu na kuathiri uhusiano wetu na Yehova. Ni nini kitakachotusaidia tuendelee kuwa macho kiroho na wenye bidii kunapokuwa na mabadiliko? Tazameni video Kubaki Imara Kiroho Unapohama, kisha mjibu maswali yafuatayo:
Ndugu mmoja alimpa baba wa familia hiyo mashauri gani?
Kanuni ya Mathayo 7:25 ilifaaje hali ya familia hiyo?
Familia hiyo ilipangaje mapema kwa ajili ya kuhama, na hilo liliwasaidiaje?
Ni nini kilichoisaidia familia hiyo kujipatanisha na mabadiliko kutanikoni na pia katika eneo?
Nimepatwa na mabadiliko gani makubwa hivi karibuni?
Ninaweza kutumiaje kanuni zilizo katika video hii kuhusu hali yangu?