HAZINA ZA NENO LA MUNGU | LUKA 10-11
Mfano wa Msamaria Mwema
Yesu alitoa mfano huo ili kujibu swali hili: “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” (Lu 10:25-29) Alijua kwamba kutaniko la Kikristo lingefanyizwa na “watu wa namna zote”—kutia ndani Wasamaria na Watu wa Mataifa. (Yoh 12:32) Mfano huo uliwafundisha wafuasi wake kwamba wanapaswa kufanya mengi zaidi ya wajibu wao ili kuwaonyesha wengine upendo, hata wale ambao ni tofauti sana nao.
JIULIZE HIVI:
‘Ninahisije kuwahusu ndugu na dada wa tamaduni tofauti na yangu?’
‘Je, mimi hupenda kuwa tu pamoja na wale ambao wana mapendezi kama yangu?’
‘Je, ninaweza kufungua kabisa moyo wangu kwa kuwafahamu vizuri zaidi Wakristo wenzangu walio na malezi tofauti na yangu?’ (2Ko 6:13)
Ningependa kumwalika nani ili . . .
tuende pamoja katika huduma
aje nyumbani kwangu kula mlo
ajiunge na familia yangu wakati wa Ibada ya Familia juma lijalo