HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YOHANA 5-6
Mfuate Yesu Ukiwa na Nia Nzuri
Yesu alipotoa mfano ambao wanafunzi wake hawakuelewa, baadhi yao walikwazika na hawakuendelea kumfuata. Siku moja tu kabla ya hapo, Yesu alikuwa amewalisha kimuujiza na hivyo kuthibitisha kwamba nguvu zake zilitoka kwa Mungu. Kwa hiyo, kwa nini walikwazika? Inaonekana kwamba nia yao ya kumfuata Yesu ilikuwa ya ubinafsi. Walikuwa wakishirikiana na Yesu ili wapate faida za kimwili.
Kila mmoja wetu anapaswa kujiuliza hivi: ‘Kwa nini ninamfuata Yesu? Je, ni kwa sababu hasa ya kupata baraka za sasa na za wakati ujao? Au ni kwa sababu ninampenda Yehova na ninataka kumpendeza?’
Kwa nini tunaweza kukwazika ikiwa hasa tunamtumikia Yehova kwa sababu zifuatazo?
Tunafurahia kuwa pamoja na watu wa Mungu
Tunataka kuishi katika Paradiso