Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 4/15 kur. 26-28
  • “Simameni Imara”—Msijikwae

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Simameni Imara”—Msijikwae
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mnyanyaso Waweza Kutukwaza
  • Mitamausho Yaweza Kudhoofisha Imani
  • Kujihukumu Vibaya Kwaweza Kuharibu
  • Usikae Umekwazwa
  • Wewe Wasimama Wapi?
  • Wewe Umekwazwa na Mambo Yaliyofanywa na Wengine?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Hakuna Kitu Chochote Kinachoweza Kuwakwaza Waadilifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Je! Wewe Unaacha Wengine Wakukwaze?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je, Utakwazika kwa Sababu ya Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 4/15 kur. 26-28

“Simameni Imara”—Msijikwae

SUALA kubwa zaidi ya yote linalokabili ainabinadamu leo ni lile la enzi kuu ya ulimwengu wote mzima. Yehova anatualika tuchukue msimamo na kuhesabiwa katika jambo hili kwa kujitiisha kwa Kristo Yesu, Mfalme mwekwa wake. Kuna uhitaji wenye umuhimu kuitikia mwaliko wake, na kwa miaka mitano tu iliyopita, watu mmoja mmoja zaidi ya milioni moja wamefanya hivyo. Lakini hawa wamepata kuona kwamba mengi zaidi yanahusika katika kuchukua msimamo kuliko kufanya uamuzi wa mara moja tu wa kutumikia Yehova. Lazima kuwe na wakfu wa muda wote wa maisha. Je! sisi tutadumisha msimamo wetu wakati mambo yanapokuwa magumu? Au tutadhoofika polepole, baada ya ‘kusimama imara’ mwanzoni?—1 Wakorintho 16:13; Waebrania 2:1.

Ikiwa wewe hukupata kuona mwendo wa Kikristo ukiwa rahisi, farijiwa kwa kujua kwamba ndivyo ilivyokuwa kwa Yesu Kristo. Ndiyo, hata Mwana mzaliwa-pekee wa Mungu alilazimika kusali apate nguvu ili adumishe msimamo wake, hasa wakati mtihani wake mgumu kuliko yote ulipokaribia. Mwone akilini mwako akiwa katika shamba la Gethsemane, akisali kwa moyo wa bidii: “Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.” (Marko 14:36) Alijua kwamba mwendo ulio mbele ulikuwa mgumu. Hasa yeye alijua kwamba jina la Baba yake lingehusika. Kwa sababu hiyo, mtu aliye mkamilifu peke yake duniani hakuona aibu kuomba msaada.

Wakati mambo yanapokuwa magumu kwetu, sisi tuna chanzo kile kile cha nguvu alichokuwa nacho Yesu. Sisi tunaweza kusali kwa Yehova kwa ajili ya msaada ili tusijikwae au kuanguka. Lakini ni hatari gani zinazoweza kujitokeza kutufanya tujikwae? Kujua hilo na kujitayarisha kimbele huenda kukatusaidia tuepuke kujikwaa.

Mnyanyaso Waweza Kutukwaza

Biblia huonya: “Wale wote wanotamani kuishi kwa ujitoaji kimungu katika ushirika na Kristo Yesu watanyanyaswa pia.” (2 Timotheo 3:12, NW) Mnyanyaso unaweza kusababisha tujikwae, nao waja kwa namna nyingi. (Marko 4:17) Huenda ukawa marufuku ya kisheria—yakileta hatari ya kifungo gerezani na hata kifo—jeuri ya wanaghasia, upinzani wenye kudhoofisha imani wa siku baada ya siku wa mwenzi wa ndoa mpinzani aliyepiga moyo konde, au dhihaka za daima za wanashule wenzi.

Ni vigumu kuvumilia mnyanyaso, lakini sisi tumeonywa kwamba utatokea kwa namna moja au nyingine. Kwa sababu hiyo, twaweza kujenga imani yetu sasa na tujifunze kutegemea nguvu za Yehova ili wakati ujapo, tutavumilia kwa nguvu hizo. (1 Petro 4:13, 14; 5:6-11) Hata hivyo, mara nyingi vikwazo ni vyenye hila zaidi ya shambulio kali la mnyanyaso.

Mitamausho Yaweza Kudhoofisha Imani

Nani asiyekumbuka hisia yenye kubomoa iliyotupata wakati sisi tulipokuwa watoto nasi tukahisi tumetamaushwa? Je! wakumbuka wakati Baba alipoahidia jamaa jambo zuri lakini kwa sababu fulani akabadili nia yake? Au wakati alipokuwa akupeleke kao la wanyama-mwitu waliofugwa na kwenye dakika ya mwisho akalazimika kufutilia mbali hilo? Jinsi ulivyotamauka!

Watu wazima walio Wakristo wanaweza kutamauka pia, na katika visa fulani hilo limeongoza kwenye msiba wa kiroho. Wengine waliweka tumaini lao kwenye tarehe fulani ambayo walikuwa na uhakika kwamba Har–Magedoni ingekuja. Wakati hakuna jambo lililotukia siku hiyo, walitamaushwa. Wengine walitamaushwa wakati pendeleo fulani walilotumainia halikupatikana. Zaidi ya hilo, watu wanaweza kutamausha. Msichana mmoja wa miaka 18 aliambia wazazi wake kwamba alitamaushwa sana na mwenendo wa baadhi ya vijana kundini—na kushindwa kwa wazazi wao kuwapa nidhamu—hata hakutaka lolote linalohusiana na ukweli.

Ingawa mtamausho unaeleweka chini ya hali hizi zote, je! inawapasa wale waliotamaushwa wakwazike na kutoka katika uhusiano wao pamoja na Yehova? Wazia mtamauko wa Yesu wakati mitume wake walipoendelea kubishana juu ya nani aliyekuwa mkubwa zaidi ya wote miongoni mwao, hivyo wakionyesha wana maoni ya kutaka makuu. (Luka 9:46; 22:24) Wazia, vilevile, mtamauko wa Ayubu wakati waandamani wake watatu waliokuwa wamekuja ili wamsaidie walipoanza kutilia shaka uaminifu wake! (Ayubu 22:5-10) Hata hivyo, Yesu na Ayubu hawakukwazika.

Binadamu wote ni dhaifu, hivyo lingekuwa jambo lisilo la akili kuruhusu kushindwa kwa wengine kuathiri uhusiano wetu pamoja na Yehova. (Zaburi 51:5) Kutokamilika kwa wengine hakupasi kutupofushe tusione kazi nzuri ajabu anayofanya Yehova anapokusanya “tena vitu vyote pamoja katika Kristo.” (Waefeso 1:9, 10, NW) Kumbuka kwamba ni binadamu wasiokamilika, wenye dhambi kama sisi ambao Yehova anakusanya, binadamu wanaohitaji nidhamu na kusafishwa ili wapate nguvu. (Zaburi 130:3) Adui yetu si ndugu yetu Mkristo asiyekamilika bali Shetani, atakaye kutumeza akiweza. Yeye hatafanikiwa ‘tukimpinga, na kuwa thabiti katika imani.’ (1 Petro 5:8, 9) Tukiwa na imani kama hiyo, sisi hatutatahayarika [hatutatamauka, NW]’ hata kidogo.—Warumi 9:33.

Kujihukumu Vibaya Kwaweza Kuharibu

Wengine wamepoteza uhusiano wao pamoja na Yehova Mungu kwa sababu ya kuhisi hawastahili. Wakifahamu udhaifu wao wenyewe na mapungukio yao, wanafikia uamuzi wa kwamba Yehova hangekubali kamwe utumishi wao. Wanahisi kwamba kwa mtu kama wao kudai kwamba ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova ni unafiki tu. Je! wewe umepata kuwa mkali kwako mwenyewe jinsi hiyo? Ikiwa ndivyo, inakupasa kupiga vita dhidi ya hisia hizo.

Je! wewe wahisi hustahili kutumikia Yehova? Basi jiulize, ‘Nani ana ustahili wa pendeleo hili kubwa?’ Wakristo wote wanapiga vita ya daima dhidi ya kutokamilika kwao wenyewe. Hata mtume Paulo alilalamika hivi: “Ninapotaka kufanya lililo jema, ubaya ni karibu nami.” (Warumi 7:21, ZSB) Je! Paulo alikuwa mnafiki kwa sababu yeye alifanya mambo yaliyokuwa makosa nyakati nyingine? Hapana. Mnafiki ni mtu ambaye hujisingizia kuwa vile asivyo. Ikiwa sisi tunajitahidi kufanya lililo sawa lakini twateleza pindi kwa pindi ijapokuwa sisi wenyewe hatupendi, je! huko ni kujisingizia juu ya jambo fulani? Bila shaka sivyo.

Biblia hutusihi ‘tuvae utu mpya.’ (Waefeso 4:24) Ingawaje, hiyo yamaanisha kwamba tunapoteza tabia zote za ule utu wa kale? Hapana. Katika barua yake kwa Wakolosai, Paulo alisema kwamba ule utu mpya ‘unafanywa upya’ kupitia maarifa sahihi. (Wakolosai 3:9, 10) Usemi ‘unaofanywa upya’ unadokeza tendo lenye kuendelea. Hivyo kugeuza utu wetu ni jambo lenye kuendelea. Basi, haishangazi kwamba pindi kwa pindi tunagundua makosa ndani yetu wenyewe.

Bila shaka, hiyo si kupunguza uzito wa dhambi, wala haimaanishi twaweza kujiachilia tushindwe na kishawishi bila kupiga vita, tukijichukulia kwamba kama kawaida Yehova atatusamehe. Lakini inatusaidia tusijichambue kupita kiasi. Na hilo linatufanya tumpende Yehova hata zaidi kwa sababu aliandaa dhabihu ya ukombozi ya Kristo ili sisi tuweze kumtumikia ijapokuwa hali yetu yenye dhambi iliyorithiwa.

Mtume Yohana alitoa oni lenye kusawazika juu ya jambo hili aliposema: “Nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi.” Ndipo akaongeza kama mambo yalivyo hakika: “Na kama mtu akitenda dhambi [kwa sababu ya kutokamilika kwa kibinadamu], tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo.” (1 Yohana 2:1) Badala ya kujihukumu vibaya kupita kiasi, muono-ndani huu wa hali yetu pamoja na msaada ambao Yehova ameandaa hutuongoza tukariri maneno ya Paulo: “Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu.”—Warumi 7:25.

Usikae Umekwazwa

Yesu alitoa onyo kali kwa yeyote ambaye angekuwa sababu ya kikwazo: “Atakayemkosesha [mkwaza, NW] mmoja wa wadogo hawa waniaminio, yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari.” (Mathayo 18:6) Lakini namna gani yule ambaye amekwazwa? Ikiwa sisi tumekwazwa na mtu fulani au hali fulani, je! yatupasa kujitolea udhuru na kusema: “Basi, si kosa langu, kwa hiyo sitatumikia Yehova tena”?

Fikiria kielezi kimoja. Je! wewe umepata kuteleza wakati wowote juu ya kipande cha barafu au ukajikwaa ulipopiga hatua? Pengine hatari hiyo ilikushtukia ghafula. Inaeleweka kwamba ulijipata mwenyewe ukiwa umejibwagaza chini. Lakini ulifanya nini halafu? Je! ulisema: “Si kosa langu kwamba nalala hapa. Ya kulaumiwa ni ile barafu [au hatua]. Hivyo sitaamka tena”? Yaelekea zaidi, ulisimama na ukatembea haraka ulivyoweza kuondoka kwenye tamasha hiyo yenye kuaibisha.

Je! haingekuwa ivyo hivyo katika mambo ya kiroho? Ikiwa twaudhiwa na hali fulani au na Mkristo fulani mwenzetu, hilo ni tatizo zito linalopasa kushughulikiwa. Hata hivyo, ikiwa sisi tunakaa tumekwazwa, tukisisitizia kulaumu mtu mwingine kwa tatizo letu, je! si kweli kwamba hali hiyo inazidi kuwa kosa letu wenyewe?

Kwa furaha, tukikwazwa, wazee na wengine waliokomaa kundini wana nia zaidi ya kusaidia. (Wagalatia 6:1) Na Yehova mwenyewe hutoa nguvu kwa wale wanaotamani kumtumikia ijapokuwa magumu. (Wafilipi 4:13) Kwa hiyo yatupasa sikuzote tuwe tayari kuomba msaada ikiwa inaelekea kwamba jambo fulani litaingilia msimamo wetu imara kwa ajili ya Yehova na Ufalme wake. Ndipo hatutampa Shetani ushindi kwa kukwazwa na kukaa tumekwazwa.

Wewe Wasimama Wapi?

Kila siku, watumishi walio wakfu wa Mungu hukabili masuala ambayo hutahini ujitoaji wao kwa Yehova. Hata washindane na nini, ni lazima wasimame na kuhesabiwa upande wa Mfalme wa Kimesiya wa Yehova. Watawala wenye nguvu wa dunia hii wamechukua msimamo wao “dhidi ya Yehova na dhidi ya mtiwa-mafuta wake.” Ni pendeleo lililoje tulilo nalo la kusimama kwa ajili yake!—Zaburi 2:2, NW.

Hata hivyo, sisi hatuwezi kusimama dhidi ya uvutano wa mfumo huu wote wa mambo kwa nguvu zetu wenyewe, hivyo tunafarijiwa na ahadi ya Yesu ya kuwa pamoja na kundi lake “mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:20, NW) Yeye atatutegemeza. Kwa kuongezea, msaada mkubwa waja wakati tunaposhikamana karibu karibu na Yehova na kutafuta utegemezo kutoka kwake. Kugeukia Neno lake kwaweza kutupa nguvu. Wakati ambao huenda tukahisi hatuwezi kuvumilia, Zaburi 55:22, NW inatualika ‘tumtupie Yehova mwenyewe mzigo wetu, naye atatutegemeza. Hataruhusu kamwe mwadilifu atikisike.’ Ndiyo, Biblia inahimiza watu wote wa Mungu ‘wasimame imara katika imani’—na wasijikwae.—1 Wakorintho 16:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki