MAISHA YA MKRISTO
Upendo Unawatambulisha Wakristo wa Kweli—Linda Umoja Wetu Wenye Thamani
KWA NINI NI MUHIMU: Usiku wa kabla ya kifo chake, Yesu alisali kwamba wafuasi wake “waunganishwe kikamili.” (Yoh 17:23, maelezo ya chini) Ili tuendelee kuwa na umoja, ni lazima tuonyeshe upendo ambao “hauweki hesabu ya ubaya.”—1Ko 13:5.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Mwige Yehova kwa kutafuta sifa nzuri za wengine
Samehe kwa hiari
Baada ya kusuluhisha jambo, usilizungumzie tena.—Met 17:9
TAZAMENI VIDEO ‘IWENI NA UPENDO KATI YENU WENYEWE’—USIWEKE HESABU YA UBAYA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Katika sehemu ya kwanza ya video, Helen alionyeshaje kwamba alikuwa ‘akiweka hesabu ya ubaya’?
Katika sehemu ya pili ya video, Helen alishindaje mawazo yake yasiyofaa na kuwa na mtazamo unaofaa?
Mwishowe, Helen alichangiaje umoja wa kutaniko?
Ni nani tunayemuumiza zaidi tunapoweka hesabu ya ubaya?