HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 2 WAKORINTHO 7-10
Huduma Yetu ya Kutoa Msaada
Wakristo wamepewa huduma inayohusisha mambo mawili —“huduma ya upatanisho,” yaani, kazi yetu ya kuhubiri na kufundisha, na “huduma ya kutoa msaada” kwa ajili ya waabudu wenzetu. (2Ko 5:18-20; 8:4) Hivyo, kuwasaidia Wakristo wenye uhitaji ni sehemu ya utumishi wetu mtakatifu. Kwa kushiriki huduma hiyo,
tunawaandalia ndugu na dada zetu mahitaji yao.—2Ko 9:12a
tunawasaidia walioathiriwa kurudia ratiba nzuri ya mambo ya kiroho ambayo inatia ndani kushiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri, jambo linaloonyesha kwamba wanathamini ukarimu huo wa Yehova.—2Ko 9:12b
tunamletea Yehova utukufu. (2Ko 9:13) Kazi ya kutoa msaada inawatolea wote ushahidi, kutia ndani wale walio na maoni mabaya kuhusu Mashahidi wa Yehova