Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Juni uku. 8
  • Lifanye Funzo Lako la Kibinafsi Liwe Lenye Kuthawabisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lifanye Funzo Lako la Kibinafsi Liwe Lenye Kuthawabisha
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kuendelea Kulishika Sana Neno la Uzima’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kupata Upendezi Katika Neno la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Funzo Lina Faida
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Funzo—Lenye Kuthawabisha na Lenye Kufurahisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
mwb19 Juni uku. 8

MAISHA YA MKRISTO

Lifanye Funzo Lako la Kibinafsi Liwe Lenye Kuthawabisha

KWA NINI NI MUHIMU: Kuwa na funzo la kibinafsi la Neno la Mungu hutusaidia “kufahamu kikamili upana na urefu na kimo na kina” cha kweli. (Efe 3:18) Pia, linatusaidia kubaki bila lawama wala doa katika ulimwengu huu mwovu na “kulishika sana neno la uzima.” (Flp 2:15, 16) Funzo la kibinafsi la Neno la Mungu linatupa nafasi ya kujichagulia habari tunazohitaji sisi binafsi. Tunaweza kufanya nini ili kutumia vizuri muda tunaosoma na kujifunza Biblia?

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tia mistari alama na uandike habari katika Biblia yako ya kujifunzia, iwe imechapishwa au ya kielektroni

  • Jiulize maswali haya unaposoma Neno la Mungu: ‘Nani? Nini? Lini? Wapi? Kwa nini? Jinsi gani?’

  • Pata habari kamili. Ukitumia vifaa vya utafiti vinavyopatikana, fanya utafiti kuhusu habari au mstari wa Biblia

  • Tafakari mambo unayosoma ili kutambua jinsi habari hiyo inavyokuhusu

  • Tumia mambo unayojifunza katika maisha yako ya kila siku.—Lu 6:47, 48

TAZAMENI VIDEO ENDELEA “KULISHIKA SANA”—KUPITIA FUNZO LA KIBINAFSI LENYE MATOKEO, KISHA MZUNGUMZIE MASWALI YAFUATAYO:

  • Watu fulani wamefafanuaje funzo la kibinafsi?

  • Kwa nini tunapaswa kuanza kila kipindi cha funzo la kibinafsi kwa sala?

  • Ni nini kinachoweza kutusaidia kuelewa vizuri zaidi simulizi la Biblia?

  • Tunaweza kuweka alama za aina gani katika Biblia yetu ya kujifunzia?

  • Kwa nini ni muhimu sana kutafakari tunapojifunza Neno la Mungu?

  • Tunapaswa kufanya nini na mambo tunayojifunza?

Dada akijifunza Biblia kibinafsi kwa kina; ndugu akitia rangi tofauti kwenye Biblia yake; dada akiwaeleza wanaume wawili habari alizoandika katika Biblia yake; ndugu akisali

“Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako! Ninaitafakari mchana kutwa.”​—Zb 119:97

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki