MAISHA YA MKRISTO
Lifanye Funzo Lako la Kibinafsi Liwe Lenye Kuthawabisha
KWA NINI NI MUHIMU: Kuwa na funzo la kibinafsi la Neno la Mungu hutusaidia “kufahamu kikamili upana na urefu na kimo na kina” cha kweli. (Efe 3:18) Pia, linatusaidia kubaki bila lawama wala doa katika ulimwengu huu mwovu na “kulishika sana neno la uzima.” (Flp 2:15, 16) Funzo la kibinafsi la Neno la Mungu linatupa nafasi ya kujichagulia habari tunazohitaji sisi binafsi. Tunaweza kufanya nini ili kutumia vizuri muda tunaosoma na kujifunza Biblia?
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Tia mistari alama na uandike habari katika Biblia yako ya kujifunzia, iwe imechapishwa au ya kielektroni
Jiulize maswali haya unaposoma Neno la Mungu: ‘Nani? Nini? Lini? Wapi? Kwa nini? Jinsi gani?’
Pata habari kamili. Ukitumia vifaa vya utafiti vinavyopatikana, fanya utafiti kuhusu habari au mstari wa Biblia
Tafakari mambo unayosoma ili kutambua jinsi habari hiyo inavyokuhusu
Tumia mambo unayojifunza katika maisha yako ya kila siku.—Lu 6:47, 48
TAZAMENI VIDEO ENDELEA “KULISHIKA SANA”—KUPITIA FUNZO LA KIBINAFSI LENYE MATOKEO, KISHA MZUNGUMZIE MASWALI YAFUATAYO:
Watu fulani wamefafanuaje funzo la kibinafsi?
Kwa nini tunapaswa kuanza kila kipindi cha funzo la kibinafsi kwa sala?
Ni nini kinachoweza kutusaidia kuelewa vizuri zaidi simulizi la Biblia?
Tunaweza kuweka alama za aina gani katika Biblia yetu ya kujifunzia?
Kwa nini ni muhimu sana kutafakari tunapojifunza Neno la Mungu?
Tunapaswa kufanya nini na mambo tunayojifunza?
“Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako! Ninaitafakari mchana kutwa.”—Zb 119:97