HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YAKOBO 3-5
Onyesha Hekima Kutoka kwa Mungu
Hekima ya Yehova inaweza kutumika katika hali zote. Kwa mfano, inaweza kutusaidia kufanya amani na waabudu wenzetu. Ikiwa tumesitawisha hekima kutoka kwa Mungu, itaonekana wazi katika matendo yetu.
JIULIZE HIVI: ‘Nimeonyesha sifa zipi hivi karibuni kati ya sifa zifuatazo za hekima kutoka kwa Mungu? Ninaweza kufanya nini ili kuonyesha sifa hizo kwa njia nzuri zaidi?’
Safi
Kufanya amani
Usawaziko
Tayari kutii
Kujaa rehema na matunda mema
Kutokuwa na ubaguzi
Kutokuwa na unafiki