Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb19 Oktoba uku. 7
  • Unalithamini Neno la Mungu Kadiri Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unalithamini Neno la Mungu Kadiri Gani?
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
  • Habari Zinazolingana
  • Waliithamini Biblia—Kisehemu (William Tyndale)
    Habari Zaidi
  • William Tyndale—Mwanamume Mwenye Busara
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Biblia ya William Tyndale Kwa Ajili ya Watu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2019
mwb19 Oktoba uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Unalithamini Neno la Mungu Kadiri Gani?

Biblia ina mawazo na maneno ya Yehova Mungu, ambaye ndiye Mtungaji wa kitabu hicho kitakatifu. (2Pe 1:20, 21) Kwa kukazia kutetewa kwa enzi kuu ya Mungu kupitia Ufalme wake, Biblia inawapa wanadamu wote tumaini kwamba maisha yatakuwa mazuri hivi karibuni. Pia, Biblia inafunua utu wenye upendo ya Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Zb 86:15.

Kila mmoja wetu ana sababu yake ya kulithamini Neno la Yehova. Lakini je, tunaonyesha kwamba tunathamini zawadi hiyo yenye thamani kwa kuisoma kila siku kisha kutumia mambo tuliyosoma maishani? Matendo yetu na yaonyeshe kwamba tunahisi kama mtunga-zaburi aliposema: “Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!”—Zb 119:97.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WALIITHAMINI BIBLIA—KISEHEMU (WILLIAM TYNDALE), KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • William Tyndale; William Tyndale akiwa kwenye matbaa yake; nakala ya toleo la kwanza la Agano Jipya la Tyndale

    Kwa nini William Tyndale alitafsiri sehemu za Biblia?

  • Kwa nini jitihada zake za kutafsiri Biblia zilikuwa za pekee sana?

  • Nakala za Biblia ya Tyndale ziliingizwaje Uingereza kisiri?

  • Kila mmoja wetu anaweza kuonyeshaje kwamba analithamini Neno la Mungu?

MAMBO YA KUTAFAKARI: Ni kwa njia gani Neno la Mungu ni kama . . .

  • taa na nuru?—Zb 119:105

  • maji?—Efe 5:26

  • upanga?—Efe 6:17

  • kioo?—Yak 1:23-25

SOMA NENO LA MUNGU KILA SIKU

Ratiba ya Usomaji wa Biblia

Je, umejaribu kutumia Ratiba ya Usomaji wa Biblia iliyo kwenye jw.org? PDF ya ratiba hiyo ina viunganishi vinavyokupeleka moja kwa moja kwenye jw.org na kukufungulia andiko unalotaka kusoma. Ikiwa rekodi za kusikiliza zinapatikana katika lugha yako, unaweza pia kuzipata kupitia jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki