MAISHA YA MKRISTO
Unalithamini Neno la Mungu Kadiri Gani?
Biblia ina mawazo na maneno ya Yehova Mungu, ambaye ndiye Mtungaji wa kitabu hicho kitakatifu. (2Pe 1:20, 21) Kwa kukazia kutetewa kwa enzi kuu ya Mungu kupitia Ufalme wake, Biblia inawapa wanadamu wote tumaini kwamba maisha yatakuwa mazuri hivi karibuni. Pia, Biblia inafunua utu wenye upendo ya Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Zb 86:15.
Kila mmoja wetu ana sababu yake ya kulithamini Neno la Yehova. Lakini je, tunaonyesha kwamba tunathamini zawadi hiyo yenye thamani kwa kuisoma kila siku kisha kutumia mambo tuliyosoma maishani? Matendo yetu na yaonyeshe kwamba tunahisi kama mtunga-zaburi aliposema: “Jinsi ninavyoipenda sana sheria yako!”—Zb 119:97.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA WALIITHAMINI BIBLIA—KISEHEMU (WILLIAM TYNDALE), KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kwa nini William Tyndale alitafsiri sehemu za Biblia?
Kwa nini jitihada zake za kutafsiri Biblia zilikuwa za pekee sana?
Nakala za Biblia ya Tyndale ziliingizwaje Uingereza kisiri?
Kila mmoja wetu anaweza kuonyeshaje kwamba analithamini Neno la Mungu?