MAISHA YA MKRISTO
Dunia ‘Ilimeza Mto’
Pindi mbalimbali katika historia, mamlaka za serikali zimewasaidia watu wa Yehova. (Ezr 6:1-12; Est 8:10-13) Na hata katika siku zetu, tumeona “dunia,” yaani, wenye mamlaka ambao wana usawaziko katika ulimwengu huu, wakiumeza “mto” wa mateso unaochochewa na “yule joka,” Shetani Ibilisi. (Ufu 12:16) Yehova, “Mungu anayeokoa,” anaamua nyakati fulani kuwachochea watawala wa kibinadamu kuwasaidia watu wake.—Zb 68:20; Met 21:1.
Vipi ukifungwa gerezani kwa sababu ya imani yako? Usitilie shaka kamwe kwamba Yehova anakulinda. (Mwa 39:21-23; Zb 105:17-20) Uwe na uhakika kwamba imani yako itathawabishwa na utimilifu wako utawatia moyo ndugu zako ulimwenguni pote.—Flp 1:12-14; Ufu 2:10.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA NDUGU NCHINI KOREA WAACHILIWAKUTOKA GEREZANI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kwa nini maelfu ya ndugu zetu walifungwa gerezani miaka iliyopita nchini Korea Kusini?
Ni maamuzi gani ya mahakama ambayo yalifanya baadhi ya ndugu zetu waachiliwe huru mapema?
Tunaweza kuwasaidiaje ndugu zetu ulimwenguni pote ambao wamefungwa gerezani kwa sababu ya imani yao?
Tunaweza kutumiaje uhuru tulio nao sasa?
Ni nani hasa anayetusaidia kupata ushindi mahakamani?
Ninatumiaje uhuru wangu mwenyewe?