HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 12-14
Agano Linalokuhusu
Yehova alifanya agano pamoja na Abrahamu, ambalo liliweka msingi wa kisheria wa Ufalme wa mbinguni
Inaonekana agano hilo lilianza kufanya kazi mwaka wa 1943 K.W.K. Abrahamu alipovuka Mto Efrati alipokuwa akielekea Kanaani
Agano hilo litaendelea kufanya kazi mpaka Ufalme wa Kimasihi utakapoangamiza maadui wa Mungu na kuziletea baraka familia zote duniani
Yehova alimbariki Abrahamu kwa sababu ya imani yake kubwa. Tukionyesha kwamba tuna imani katika ahadi za Yehova, tunatarajia kupata baraka gani zinazotegemea agano ambalo Mungu alifanya pamoja na Abrahamu?