MAISHA YA MKRISTO
Uwe Mnyenyekevu Unaposifiwa na Wengine
Nyakati nyingine, huenda wengine wakatusifu, au kutupongeza. Hilo linaweza kututia moyo hasa ikiwa wanatusifu kutoka moyoni na kwa nia nzuri. (Met 15:23; 31:10, 28) Lakini tunapaswa kuwa waangalifu kwamba hilo lisitufanye tujihisi kuwa bora kuliko wengine na kuwa na kiburi.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UWE MSHIKAMANIFU KAMA YESU—UNAPOSIFIWA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Huenda watu wakatusifu kuhusu mambo gani?
Akina ndugu walimsifu Sergei kwa njia gani?
Walimsifuje kwa njia isiyofaa?
Umejifunza masomo gani kutokana na jinsi Sergei alivyojibu kwa unyenyekevu?