HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 10-11
Musa na Haruni Waonyesha Ujasiri Mkubwa
Musa na Haruni walionyesha ujasiri mkubwa walipozungumza na Farao, aliyekuwa mtu mwenye nguvu zaidi ulimwenguni wakati huo. Ni nini kilichowawezesha kufanya hivyo? Biblia inasema hivi kumhusu Musa: “Kwa imani aliondoka Misri, lakini hakuogopa hasira ya mfalme, kwa maana aliendelea kuwa imara kama mtu anayemwona Yule asiyeonekana.” (Ebr 11:27) Musa na Haruni walikuwa na imani yenye nguvu katika Yehova na walimtegemea.
Ni hali zipi ambazo unahitaji ujasiri kumweleza mtu mwenye mamlaka imani yako?