HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 37-38
Madhabahu Katika Hema la Ibada na Fungu Lake Katika Ibada ya Kweli
Madhabahu zilizokuwa kwenye hema la ibada zilijengwa kulingana na maagizo ya Yehova na zilikuwa na maana ya pekee.
Kama kufukiza uvumba uliochanganywa kwa ustadi, sala zinazokubalika zinazotolewa na watumishi wa Yehova zinampendeza
Yehova alikubali dhabihu zilizotolewa juu ya madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa. Kuwepo kwa madhabahu hiyo mbele ya patakatifu kunatukumbusha kwamba ni muhimu kuwa na imani katika dhabihu ya fidia ya Yesu ili tupate kibali cha Mungu.—Yoh 3:16-18; Ebr 10:5-10
Tunaweza kutayarishaje sala zetu kama uvumba mbele za Mungu?—Zb 141:2